SHINEY-SHOULD THE GANGSTAR APOLOGISE??/// Wengi wamemzoea kwa mtindo wake wa rnb na afro-fusion ila binti huyu anayetokea papa hapa mjini Mombasa amezuka na mtindo kwa wimbo mpya wa hiphop.Shiney aliyetokea kwa mara ya kwanza kabisa ndani ya BIGFOOT PRODUCTION na kuvuka mipaka ya pwani kusajiliwa SIMAMA RECORDS Nairobi alikusudia kufanya wimbo mtindo wa hiphop baada ya tukio flani lililomkosanisha na msanii gwiji wa hiphop hapa pwani.Kudhihirisha kuwa anao uwezo wa kurap,Shiney Anne alijitosa kwenye maji makuu ya hiphop na kuwatayarishia mashabiki zake wimbo GANGSTAR APOLOGY.Wimbo huo uliandaliwa chini ya talanta yake produza mahiri na stadi Baindo ambaye pia ni CEO wa Bigfoot production.Tulijaribu kuwasiliana na produza Baindo alitueleza kuhusu project hio ya GANGSTAR APOLOGY,hivi ndivyo alivyosema,"Kusudio la binti Shiney kuandaa wimbo kwa mtindo wa hiphop ilikuwa ni kutaka kupata mashabiki zaidi na kudhihirisha uwezo wa talanta yake.Wimbo upo tayari na mashabiki wautarajie hewani dakika yoyote kuanzia leo." Utunzi wa wimbo huo ni wa hali ya juu na kweli msanii Shiney amedhihirisha uwezo wa kurap kando na kuimba tu.Nadhani itakuwa vyema zaidi tukimpa jina la SHINEY THE HIPHOP QUEEN!! Wacha tusimalize utamu,ukiskia utakumbuka tulivyokueleza!!

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!