LAWAMA KUBWA KWA WASANII WA PWANI

Kila mara tunasikia washika dau wa muziki wa pwani hasa mapromoter na maproduza wakilalamika na kuwakashifu kwa ukali baadhi ya wasanii. Hii imebainika wazi kuwa wasanii hawana shukrani kamwe na wamejawa na viburi,sanasana wale wanaosikika kwenye maredio na wanaopiga show.
Musa Babaz

Juzijuzi kwenye kituo flani cha redio hapa pwani,promota ambaye vilevile ni meneja na event organiser MUSA BABAZ aliongea hewani kwa kejeli na chuki kuu maneno haya......'Wasanii ndio watu ambao hawajui fadhila au utu katika hii dunia.Ni wepesi wakusahau na wingi wa kiburi pindi wanapofanikwa baada ya kusaidiwa........' Tulijaribu kuwauliza baadhi ya washika dau wawili watatu wa muziki wa pwani kama kweli wanakubaliana na maneno hayo.
Wilberforce wa Heartbeat



PROMOTER WILBERFORCE WA HEARTBEAT........"Yeah, cz kama mimi na kampuni yangu Heartbeat ent nishawasaidia wasanii wengi tu ajabu ni pale milango inapofunguka,hata simu wala sms ya shukrani sijapata kutoka kwa hata mmoja wao..thats why naunga mkono unaposema wasanii ni wepesi wa kusahau na wingi wa kiburi pindi wanapofanikiwa baada ya kusaidiwa......." 
 
Produza Baindo


PRODUZA BAINDO WA BIGFOOT PRODUCTION NAYE ALINENA HAYA........."Wasanii huja studio bila hela na kwa sababu produza anataka sana kukuza vipaji anawaacha kufanya kazi bure,wasanii hao hao wanaposaidiwa hawatulii kamwe wanaenda kwa studio tofauti tofauti kulialia ili waweze rekodi muziki bure.Vilevile msanii anapoanza kufanikiwa anavunja heshima yake na produza aliyemtoa kwa jasho lake.Kiburi kinamvaa na kujiona supasta kwa sababu ya kupewa nafasi ya kufanya mziki bure studio tofauti tofauti.Jambo hili linaudhi na kamwe halijengi sanaa ya 
pwani........" 
PRODUZA KHALID WA A MILLION RECORDZ NAYE ALIYARUDIA MANENO YALE YALE YA MUSA BABAZ......'Wasanii ndio watu ambao hawajui fadhila au utu katika hii dunia.Ni wepesi wakusahau na wingi wa kuburi pindi wanapo fanikwa baada ya kusaidiwa........' 
Haya si maneno yangu,muulizeni Musa Babaz alimaanisha nini. Langu ni jicho tu....."
 JE WASANII MTAJITETEA VIPI? MNALO LA KUSEMA?

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!