PWANI TV KUANZA KUPEPERUSHA VIPINDI HEWANI!!


 Baada ya kujibu maombi ya wanapwani kutaka stesheni yao,Pwani TV ilianzishwa mwaka huu mwezi uliopita kukata kiu cha watu wa pwani. Ilipoanza Pwani Tv ilichukua muda kabla ianze rasmi kuonyesha vipindi tofauti tofauti na hapo jana ilitangaza rasmi kuwa vipindi vitaanza kuonyeshwa wiki hii.
Tukinakili waliyopachika kwenye ukurasa wao wa facebook...'Mpwani upo!!! Tunachukua fursa hii kukujulisha mwanzo wa kupeperusha hewani vipindi vyakusisimua, habari zinazokulenga na kukuhusisha wewe kama Mpwani. Vipindi vya kuangazia elimu, biashara, afya, michezo na burudani tosha la kukutumbuiza vilivyo. Juma ni hili, siku ni ya jumatano. Usiwachwe hamnazo bandarini kwani meli yang'oa nanga...."

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!