PATA KUMFAHAMU POUL IBRAHIM KWENYE ULINGO WA MODELING.



Pwani Usanii: Jina lako wajulikana kama nani?

Poul Ibrahim:Poul Ibrahim

PU: Tueleze kiasi kuhusu maisha yako ya utotoni.

Poul Ibrahim:Nilizaliwa Likoni,mitaa ya Kiwerera pale Karibu na flats. Nikasomea Likoni Muslim primary na kujiunga na Pwani secondary school.
Hapo ndipo nilianza kufanya uigizaji kwenye tamasha za drama na music.

PU:Vyema kabisa. Katika uigizaji labda ulipendezwa na nini?

Poul Ibrahim: Nilipendezwa sana na vile nilivyokua najieleza mbele ya umati na vilevile nilikua dancer mkali sana.

PU:Na labda ulianza lini mambo ya modeling?


Poul Ibrahim: Modeling nilianza high school ila sikua serious serious sana hadi nilipomaliza shule kwa sababu ya masomo.
Nilipomaliza masomo hapo ndipo nilipojimwaga uwanjani.


PU: Wewe kama model wa kiume umefanya mambo kama yapi?

Poul Ibrahim: Nimekua kwenye mashindano na tamasha tofauti za modeling na vilevile nishakua kwenye advertisements za kampuni moja-mbili hivi.

PU: Lengo lako kuu hasa ni nini?

Poul Ibrahim: Lengo langu kuu ni kuhasisha watu kuwa modeling kwa wavulana pia ipo na ukitia bidii unaweza fanikiwa.

PU: Shida gani unazopitia kama model wa kivulana?

Poul Ibrahim: Shida ninazopitia au tunazopitia kama models wa kiume ni kupata watu wanaothamini kazi yetu,kwa sababu watu wamezoea models wa kike pekee.

PU: Labda mtu akitaka kukufikia anaweza kupata vipi?

Poul Ibrahim: Anaweza kunipata kupitia Facebook Poul Ibrahim au kupitia nambari yangu 0704 40 69 97.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!