HUBA MAHABUBA!!!!! STORI YA MSANII BEKA THE BOY NA MPENZIWE YAVUJA!!!!


HUBA MAHABUBA!!!!! STORI YA MSANII BEKA THE BOY NA MPENZIWE YAVUJA!!!!!!


Sanasana kwenye pitapita mitandaoni ndani ya account ya Beka ya fesibuku hutokosa kuona picha kadhaa za wawili wapendao,ambapo ni Beka na binti Fulani wa kizungu.
Jambo hili lilitufanya kuingia chini ya carpet na kupeleleza zaidi kabisa.Hapo ndipo tulipokutana na Bi. Francesca mpenziwe msanii Beka.

Baada ya maswali mawili matatu Francesca alifunguka na kutueleza kuwa alipatana na Beka mwaka kama mwaka mmoja na nusu uliopita katika tamasha la Extravaganza lililofanyika ndani ya La Rosada beach , Malindi.Wakati huo Beka alikuwa jukwaani akidondosha wimbo wake "Mtoto Wa Ghetto."
"After that we start getting in touch as friends do...and was for quite long time since my eyes changed and started to look at him with other eyes!The guy was very polite and mostly he was not showing interest for me!We got closer day by day!The voice was killing, the heart was clean, the manners were gentle and soft!!!It was like when u cut an apple and then u try to combine again the two half of that...Perfect!!
"Siwezi Juta." Alieleza Francesca.

Binti huyu alieleza kuwa nyimbo nyingi za Beka hupata ushawishi na mwelekezo kutokana na mahaba yao na jinsi yalivyojengeka. Vilevile kando na hayo yote,kama kawaida kila uhusiano huwa na vikwazo vyake na hili pia halikosi.
Baadhi ya mambo magumu ya penzi hili ni kuwa Francesca ni meneja wa Beka kimuziki hivyo basi lazima ampangie mipango yote ya muziki. Jambo hili saa zingine huleta utofauti kwani Francesca ni mwanamke anayependa jambo lifanyike atakavyo yeye na hulitaka liwe asilimia moja vyema kusiwe na kasoro zozote.
Kukikoseka lolote tu basi lawama huibuka. Hata hivyo yote tisa kumi ni kwamba wawili hawa kamwe hawatikisiki na kila uchao basi mahaba yao yanazidi kung'aa.
Baada ya kuwachia video ya "Niko Low",Francesca na msanii wake au tuseme tu mpenzi wake wapo katika harakati za kuachia video mpya kabisa kwa jina " siri ya moyo" ambapo Beka the Boy amemshirikisha Kiwanja.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!