Posts

Showing posts from March, 2017

PATA KUMFAHAMU POUL IBRAHIM KWENYE ULINGO WA MODELING.

Image
Pwani Usanii: Jina lako wajulikana kama nani? Poul Ibrahim:Poul Ibrahim PU: Tueleze kiasi kuhusu maisha yako ya utotoni. Poul Ibrahim:Nilizaliwa Likoni,mitaa ya Kiwerera pale Karibu na flats. Nikasomea Likoni Muslim primary na kujiunga na Pwani secondary school. Hapo ndipo nilianza kufanya uigizaji kwenye tamasha za drama na music. PU:Vyema kabisa. Katika uigizaji labda ulipendezwa na nini? Poul Ibrahim: Nilipendezwa sana na vile nilivyokua najieleza mbele ya umati na vilevile nilikua dancer mkali sana. PU:Na labda ulianza lini mambo ya modeling? Poul Ibrahim: Modeling nilianza high school ila sikua serious serious sana hadi nilipomaliza shule kwa sababu ya masomo. Nilipomaliza masomo hapo ndipo nilipojimwaga uwanjani. PU: Wewe kama model wa kiume umefanya mambo kama yapi? Poul Ibrahim: Nimekua kwenye mashindano na tamasha tofauti za modeling na vilevile nishakua kwenye advertisements za kampuni moja-mbili hivi. PU: Lengo lako kuu hasa ni nini? Poul Ibrahi

EXCLUSIVE STORY: THE REVELATION OF KIWANJA!!!!

Image
Kiwanja is a hip hop artiste from Malindi who has done thematic and positive music over decades. Having released hit after hit, his talent was unearthed to the bigger audience when he released Bonde chafu, that almost everyone could recite the lyrics to. He is popularly known for hit songs; Hatari (which he delivers blending both southern rap and hardcore hip hop elements) Mikono juu, 411, Baby, Siri yangu, Story zetu among other collaborations. Kiwanja has worked with top Kenyan artistes for singles like The Cypher that featured Sharamaa and Richie rich (Gurugang), Hela featuring Kaligraph Jones. Recently, he has been featured in a new music single by Beka the Boy tittled Siri ya Moyo. He is now working to release a compilation album The Genesis with his label mates at Malindi Records and a tour in different parts of the country Kenya Inspiration story.His current project mabavu is doing well in the local coastal music charts. He draws his music inspiration from his surro

MSANII DONI ATEMANA NA LEBO YA ISLANDLOVE RECORDS!!!!!!!

Image
MSANII DONI ATEMANA NA LEBO YA ISLANDLOVE RECORDS!!!!!!! Mfalme wa muziki wa Lamu,Doni ametemana na Lebo yake ya ISLANDLOVE RECORDS ndizo habari zinazotamba kwa sasa. Doni aliyesajiliwa kwenye lebo hiyo na kufanya vibao vingi vilivyofanya vizuri alikua kwenye pilka pilka za kuandaa video ya nyimbo I am original ambapo mambo yalienda ndivyo sivyo na kuleta utengamano huo. Tulipowasiliana na meneja wa Islandlove records alitueleza hivi.............." Doni gave us a big budget of his Iam original video , which was to cost a budget of 500 k which was to be done by a famous Kenyan director. We could not handle such or more than that so we had to let him go.He is an ambitious person and we wish him all the best." Hayo ndiyo maneno ya aliyekuwa meneja wa Doni na kwa sasa msanii huyu yuatafuta usimamizi mpya.

BEKA THE BOY KUWACHIA VIDEO YAKE IJUMAA HII.

Image
Beka the Boy,msanii tajika anayetokea Malindi ataachia video yake ijumaa hii. Beka aliyeandaa video yake ya wimbo 'Siri ya Moyo' chini ya director Marvin Brudaz alituhakikishia kuwa video hiyo itakuwa moto wa kuotea mbali kwani kando na kuiandaa kwenye hoteli za kifahari mbalimbali director alitumia vyombo vya kisasa ili kufanikisha malengo yake. Usikae mbali......

JE NI DHARAU AMA KEJELI???? CHIKUZEE AAMBIWA AVUE VIATU STUDIO YA DIAMOND HUKU WENZAKE WAMEVAA!!!

Image
Baada ya Chikuzee kuwachia picha akiwa studio za WCB ENTERTAINMENT ya Diamond,wengi walizikejeli kwa kuwa Chikuzee alionekana kuwa mguu chuma huku wenzake wamevaa viatu. Swali ni je,Chikuzee aliambiwa avue viatu ili asiingize vumbi lake la Likoni humo? Au je alipendelea mwenyewe kuvua viatu? Na je mbona wenzake hawakuvua viatu na yeye alivua?

CHIKUZEE KUSAJILIWA WCB YA DIAMOND??

Image
CHIKUZEE KUSAJILIWA WCB YA DIAMOND???? Habari zinazotufikia kwa sasa ni kwamba kuna fununu au tetesi ya kuwa msanii gwiji wa hapa pwani Chikuzee huenda ikiwa amesajiliwa lebo kubwa ya muziki WCB. WCB ambayo ni kampuni ya mwanamuziki Diamond platnumz ndiyo kubwa kabisa Afrika Mashariki na katika pitapita zetu mitandaoni tulipata kuona picha kibao tu kwenye account ya Chikuzee alizopiga akiwa kwenye anga za ofisi za Wasafi Classic. Chikuzee aliachia picha kadha wa kadha akiwa ndani ya ofisi na studio za WCB na vilevile akiwa na Produza tajika wa Tanzania. Hivi je msanii huyu amesajiliwa WCB??????

ADILI TOZY AFANYA MAANDALIZI YA VIDEO YAKE.

Image
ADILI TOZY AFANYA MAANDALIZI YA VIDEO YAKE. Baada tu ya kujitambulisha kimuziki,msanii anayeibukia kwa kazi,Adili Tozy ameamua kuwaburudisha mashabiki kwa video ya wimbo wake 'Acha niseme'. Nyimbo hiyo iliyotayarishwa na producer Lameck Boy inazungumzia swala linalokumba jamii na maudhui ya elimu na umaskini yamedhihirika vyema na kupewa kipao mbele. "Niliona itakuwa jambo la busara iwapo nitawachia audio na kuwabamiza mashabiki zangu kwa video juu kwa juu.Japo bado nipo katika hali ya kukita mizizi pwani,sitalegeza kamba kamwe kwa sababu nimepata management inayonipa motisha na msukumo wa kufanya kazi pasipo shida yoyote." Alieleza Adili Tozy. Video ya wimbo 'Acha niseme' uliandaliwa na kampuni ya Coastline photography and videos wikendi iliyopita na kampuni ya Remuked entertainment inayomsimamia msanii huyu imeahidi kuachia video hiyo kipindi cha wiki mbili zijazo.

WILLY M TUVA HASAIDII LOLOTE ! MSANII AANDIKA BONGE LA UJUMBE!! SOMA HAPA!!

Image
Msanii kwa jina Lang Katalang amekuja vinoma na kumkashifu mtangazaji wa Citizen wa kipindi cha Mambo Mseto na Mseto East Africa kuwa ana mapendeleo na kamwe hasaidii wasanii wanaoibuka. Lang Katalang alimpasha Mzazi Willy M Tuva kupitia account yake ya Facebook na kusema kuwa amejaribu sana awezavyo kufikisha muziki wake kwenye kipindi hicho ila juhudi zake uambulia patupu. Cheki screenshots za account ya Lang Katalang hapa -- >>>

NIKO LOW LYRICS BY BEKA THE BOY

Image
SONG:NIKO LOW ARTIST:BEKA THE BOY PRODUCED BY:SANGO(MALINDI RECORDS) VERSE 1 Kuna muda mwingine huwa Mimi natakaga Kuwa na wewe kabisa Lakini ndivyo hivyo huwa wewe unanimwagaaaaeehh Unanifanya mpaka ghetto mi natorokaga mpaka naachana ni visaa ili nipate tu ruhusa ya kukuonaga Ila kwanini umejaza hisia penzi umelitia ila Nyingi fikira zitafanya mpaka taira BRIDGE: Penzi la vurugu rugu mi siwezi Mbona unanipa uchungu na stress Penzi la vurugu rugu mi siwezi Mama aaahhh CHORUS ×2 Niko low low Niko low low Niko low low Niko low low Niko down low Niko low low Karibu unitulize Tutulize moyo VERSE 2 Nahitaji kuwa nawe ili nikuweke ubavuni mwangu Hisia zangu zielewe nikupe chochote kutoka kwangu Hakuna ajuaya mapenzi zaidi ya Romeo na Juliet Ningeweza ngefanya bajeti Mambo ya gazeti,mi siwezi Penzi la kubahatisha,mi siwezi Kukimbizana makilo mita Mi siwezi BRIDGE ×2: Penzi la vurugu rugu mi siwezi Mbona unanipa uchungu na stress Penzi la vurugu r

EXCLUSIVE INTERVIEW: KWA MARA YA KWANZA KABISA KUTANA NA MSANII ADILI TOZY!

Image
Pwani Usanii kama kawaida hupata fursa ya kuvitambulisha vipaji vipya na raundi hii tunawaletea msanii Adili Tozy aliye chini ya Remuked Entertainment. Soma zaidi..... Pwani Usanii:Tuambie jina lako la serikali na jina lako la kisanii. Adili Tozy:Jina langu la kitambulisho ninalotambulika nalo ni Ismail Chimwana Kahindi na la kikazi au nikipanda steji wananiita Adili Tozy. Pwani Usanii:Swadakta kabisa. Je ulisomea wapi? Adili Tozy:Nilisomea Kikambala primary school na kujiunga na sekondari ila Sikumaliza sekondari kwa sababu ya shida za kifamilia. Pwani Usanii: Ni kitu gani kilichokufanya kuanza muziki? Adili Tozy:Kitu kilichonifanya nianze muziki ni kuwa niliona wadogo zangu wakipaa na kufanikiwa kimuziki nami nikaamua kujitosa kwenye ulingo uo huo kwa sababu tayari kipaji nilikua nacho. Pwani Usanii: Je wafanya muziki aina gani? Adili Tozy: Nafanya muziki aina nyingi kwa sababu nina kipaji,naweza flow na mdundo wa aina yoyote. Ila kwa sasa napiga muziki wa malo

KARIBU MOMBASANI VIDEO LAUNCH JUMAMOSI HII.

Image
KARIBU MOMBASANI VIDEO LAUNCH JUMAMOSI HII. Ni tamasha la kuiwachia rasmi video ya Karibu Mombasani litakalofanyika Jumamosi hii. Tamasha hili linaloitwa Shots and Bikini pool litafanyika Reef Hotel mida ya saa tatu usiku hadi jogoo litafune mswaki. Wanamuziki Benso,GeeGee na Kigoto watafanya bonge moja la perfomance na Wanamitindo Ria Saburi na Zerina watakua kwenye mic wakiwakaribisha kila mmoja atakayewasili. Photography itafanywa na Kasino Underwater photography na deejays kama Dj Mr T Dj Electric Dj Tally Dj Saye Dj Kanja wakuwepo. Hivi kwanini ukose? Fika bila kuchelewa!!!!! Endelea kucheki video hapa - >>> https://youtu.be/NRvHG79vWE4