'MACHO' WASANII WA LAMU TAYARI KUANGASHA VIDEO KWA MARA YA KWANZA.


Waliamua kujitumbukiza kwenye kina cha maji marefu na wasanii kwa uwezo wao na weledi wa uimbaji bado wanaelea.
Wasemavyo wahenga,ukiona vyaelea bila shaka vineundwa.
Hivyo basi Producer msanii Doni na Man Azzer wanaowakilisha ISLANDLOVE RECORDS iliyopo Lamu wamekamilisha video yao ya wimbo MACHO.
Tukiwasiliana na meneja wa studio,alituleza kuwa video hiyo iliwagharinu zaidi ya elfu hamsini na mvuto wake na quality ni za hali ya juu.
"Nikitaka wasanii wangu waweze kuonyesha ulimwengu mzima kuwa kando na utalii Lamu, vipaji vipo na mandhari kabambe yenye mvuto asilia wa kipwani udhihirike." Alitueleza meneja.
Video ya macho ipo tayari kabisa na itawachiliwa hewani tarehe 11 mwezi huu.
Video hiyo ilitayarishwa na mwelekezi kwa jina XomoBoss.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!