CHIPUKIZI WA SANAA ASHTUA KWA VIDEO MPYA

CHIPUKIZI WA SANAA ASHTUA KWA VIDEO MPYA!!!

Baada tu ya kujitambulisha kwenye tasnia ya sanaa,msanii mpya Norry Classic ameamua kutolegeza kamba. Norry,aliye chini ya usimamizi wa Wapishi records amekuja vikali na kuandaa video yake ya wimbo "Ninavyokupenda" aliomshirikisha Lucky wa Kwanza.

" Karne hii ya sasa,msanii bila video basi ataambulia patupu ndiposa nikawa juu chini kutafuta video ya wimbo wangu.Nimepata usaidizi kutoka kwa marafiki na mashabiki wanaoufagilia muziki wangu ili kufanikisha haya yote. Wapishi records Vilevile ni nguzo yangu kuu katika matayarisho yote haya." Alieleza Norry.
Video hiyo itaachiliwa hivi karibuni ikifuatiwa wa audio sambamba.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!