SIRI YAVUJA....HIVI JE KILA REDIO STESHENI HUWA NA WASANII WAKE WA KUCHEZA HAPA PWANI?(part 1)


Kumbe siri ya kufifia kwa Sanaa ya pwani si kubaniwa na washika dau wa Nairobi, kutopata
show, kulaghaiwa na mapromota au mZiki quality mbovu!!? La hasha! Imebainika wazi kuwa swala
nyeti linalofanya wasanii wa pwani kufifia ni migawanyiko ya airplay au ukipenda unaweza
sema 'kila mtu na mtuwe'.

Ni Mara nyingi mashabiki wa msanii Fulani wanapoomba request na presenter kudai hana nyimbo hio ama hata pia kamwe hamjui msaniihuyo. Kuongeza msumari moto kwenye kidonda badala ya presenter ajaribu kuutafuta wimbo huo ama msanii mwenyewe ndiposa aweze mtambusha na kuwapigia mashabiki wimbo wake, presenter analaza damu na kuwacha talanta ya mwenziwe kupotea.
Jambo lengine la kushangaza ni pale msanii Fulani Ni supasta stesheni Fulani kwa kipindi Fulani na hajulikani kabisa kwa stesheni jirani. Vilevile tukirusha dongo kali kwa wasanii tabia ya kusambaza muziki wako kwa stesheni moja pekee unayojulikana so vyema. Hii inadunisha kabisa na kukuvuta chini kama msanii unayekua.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!