JE NI KWELI NZUMARI AWARDS ZITAKUWA ZA GOSPEL PEKEE? N'GAMUA UKWELI HAPA!



Baada ya tuzo za Nzumari zifanyikazo hapa pwani kupatwa na msukosuko na kutofanyika kwa miaka miwili mtawalia, mashabiki na washika dau wa tasnia ya muziki kanda ya Pwani walijiuliuza maswali mengi bila kupata majibu. Hivi majuzi baada ya mwanzilishi wa tuzo hizo Eve Adhiambo kuokoka na kumpokea Yesu kristo kama mwokozi wa maisha yake. Alikuja wazi wakati alipokuwa anahojiwa ndani ya Baraka fm na Dj Lenium na kusema kuwa tuzo za Nzumari zitafanyika ila wakati huu zitakuwa za gospel. Sababu kuu ya tuzo hizi kugeuzwa kuwa za gospel, Eve alidai kuwa ameamua kumtumikia Mungu na hii ndio njia moja ya kumtumukia. Binti huyu vilevile alidai kuwa bado yupo kwenye biashara za kuandaa matamasha. Juzi alikuwa na show moja ya kukata na shoka aliyomualika "malaika" si kutoka mbinguni Bali Nairobi kwa jina Corazon Kwamboka. Cha msingi ni kuwa kuna uwezekano mkubwa tuzo hizi za Nzumari gospel Awards kufanyika mwezi Aprili ndivyo alivyomalizia mwanadada Eve. 

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!