WASANII WATANO WA PWANI WALIOSINGIZIWA KUWA ILLUMINATI: pata ukweli hapa!

Huku sanaa ya pwani ikizidi kunawiri, miaka miwili, mmoja au hata miezi michache iliyopita wasanii wenye vipaji toka pwani walioinuka na kuipiku sanaa ya Afrika mashariki. Wasanii hao walisingiziwa kuwa katika kundi la waabudu shetani au ukipenda illuminati(kama wengi wanavyoliita)
 Baadhi yao ni: 

 1.KIDIS Kidis Nesphory Simbiga au ukipenda 'The Jembe' 
Alichipuka kwa kasi na kufanya remix ya wimbo wake 'kamua leo' ndani ya studio za grandpa records Nairobi. Hapo alipata umaarufu mkubwa mno na show nyingi zilifuata. Kilichotanda magazetini na mitandaoni ni kuwa Kidis yupo illuminati. Msanii huyu alipuzilia mbali madai hayo.  

2.CANNIBAL 
Alipojiunga na Prezzo na kutoa kibao MY CITY MY TOWN fununu ziligonga mitaani kuwa amejiunga na illuminati. Canninbal kiupande wake hakuongea lolote kuhusu madai hayo.Kimya chake kilikuwa jibu la kutosha. 

 3.ROJO-MO 
Rojo mo japokuwa hakusemwa sana, kuna uvumi ulioenea kuwa yupo katika kundi la illuminati. Katika wimbo wake HAWAJUI aliomshirikisha Totti. Rojo amekuja wazi na kurap kuwa kuna watu walisema kuwa eti yeye ni illuminati ila vilevile Rojo aliwajibu kuwa bidii ndio kila kitu na hawajui Rojo muziki anafanya kwanini. 

3.LYPSO
 Baada ya video ya SIZE YANGU Lypso aliandamwa na scandal za kila aina eti yeye ni illuminati. Alitupilia mbali madai hayo na hakusita kutoa hotsong nyingine. 

4.DADDY Q 
Alipohamia Nairobi, daddy Q alipata umaarufu haraka na bila shaka uvumi ukaanza. Daddy Q alisingiziwa kuwa illuminati jambo lililomfanya afukuzwe mazishini kwa babake wakidai kuwa yeye ndio chanzo cha babake kuaga. Q hakufa moyo bali aliyapuuzia mbali madai hayo na kuendelea kukaza buti kwenye fani ya muzikiz. 

5.KIGOTO 
Japo bado mchanga kwenye ulingo wa sanaa ya pwani; Kigoto tayari alishapakwa tope kuwa illuminati. Hii ni baada ya kujiunga na kundi la mishemishe empire linalomilikiwa na susumila na pindi tu alipojiunga nyanyake akafariki, binadamu kawaida ni walewale wakasema kuwa hayo ni matokeo ya illuminati. Kigoto aliyapuzilia mbali madai hayo na kuendelea kufanya muziki kwa wingi.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!