Exclusive! NYOTA NDOGO KUELEKEA WASHINGTON DC,USA KWA FESTIVAL YA MUZIKI PAMOJA NA WASANII WENGINE!

 Binti mzawa wa pwani ambaye wengi wanamuita mama wa muziki wa pwani,Nyota Ndogo ana tabasamu kubwa kwa kupata nafasi ya kwenda kwa tamasha la kimataifa litakalofanyika Washington Dc USA.Festival hio ambayo ni ya wanamuziki wa kizazi kipya wanaoweza kuimba live na band itakuwa ya siku kumi na tano na Nyota Ndogo ni baadhi ya arubaini waliochaguliwa kufanikisha tamasha hilo.Tuliwasiliana na Nyota Ndogo na alitueleza hivi....
"Hii jumamosi nitakua naondoka Kenya kuelekea USA kwenye festival kubwa inayokwenda kwa siku kumi na tano.Mimi ni msanii mmoja kati ya arubaini na tano waliochaguliwa kuwakilisha kenya and i'm pround nimetoka mombasa.Mimi suzana owiyo,Eric wainaina,Musaimo,Idd­ achieng,wale wanamziki wa afro pekee,tupo wengi tu ila kikubwa najivunia kuwa natoka mombasa.Tutakua huko kwa mwezi mzima tukifanya tour sehemu tofauti tofauti za nchi hio..." Twamtakia kila la kheri Nyota Ndogo anapokwenda kuiwakilisha pwani kimataifa na kweli amepatia wasanii wengine mfano mzuri.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!