SUSUMILA NI MCHAWI, CHIKUZEE ADAI.


Msanii kutoka Number one records CHIKUZEE amezidi kumukashifu vikali mwenzake Susumila kwa kudai eti yeye hufanya uchawi ili aweze kuepuka ushindani katika sanaa ya muziki wa pwani na amejaribu sana kumuroga ili aweze kuporomoka kimuziki na hata kuweza kumuroga na kumusabababishia ajali nne za barabarani ambazo aliweza kunusurika. Chikuzee aliweza kuthibitisha madai yake kwa kusema kwamba Susumila chumbani kwake yuko na kiti cheupe ambacho hua haruhusu mtu yeyote kukikalia isipokua yeye mwenyewe na pia nyumba yake imejaa ishara kibao za kishetani ambazo hua haruhusu mtu kuguza. Chikuzee Alimalizia kwa Kusema kwamba Susumila sio mtu Poa manake ana roho mbaya na amejaa na ubinafsi. Susumila nae kwa upande wake ametupilia mbali madai hayo na kusema chikuzee ni baadhi ya watu wasiopenda mafanikio yake.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!