Posts

Showing posts from February, 2015

FIDEMPA BILA SHAKA AMEIPEPERUSHA BENDERA YA DANCEHALL PWANI JUU KABISA

Image
Alitoka Pwani akiwa kinda kwa ulingo wa muziki na kuelekea Uganda kubahatisha bahati yake.Huku nyuma kila shabiki aliwachwa roho juu na kumtakia kila la kheri kwa njia aliyoichukua.Haikumakiza hata mwaka msanii wa ragga na dancehall Phidempa alipovunja ufuo na kutiririsha vibao vikali na vya kusisimua na kuchukua nafasi kula mkeka mmoja na wakali wa Afrika mashariki.Hivi majuzi bingwa huyu ambaye mizizi yake ya muziki iliota hapa Pwani alitoa kibao akishirikiana na Proff na kikafanya vyema sana.Hivi saa video yake DANGEROUS inachafua charti za muziki wa Afrika mashariki.

UNDEPICTED FILM AND PHOTOGRAPHY WAKALI WA KAZI SAFI ZA VIDEO.

Image
Miaka iliyopita kazi za wasanii wa pwani hasa video zimedhalilishwa mno na watu tofauti ila wakati umefika sanaa ya pwani kupewa sifa zake.Chini ya weledi na ujuzi wake Marvin Y. Brudas video za hali ya juu zinazopendeza kwa rangi,mvuto na teknolojia ya kisasa tayari zipo mitaani,mitandaoni,madukani na kwenye runinga zetu.Gwiji huyu aliye na ujuzi mkali ndiye anaye zitengeneza kazi hizi kwa kudirect,kushoot na kued it chini ya kampuni ya UNDEPICTED FILM AND PHOTOGRAPHY.Kampuni hii inayoenda sambamba na MALINDI RECORDS imedhihirisha uwezo wake kwenye video ya msanii Katoi wa Tabaka wimbo ukiwa "fly" akishirikiana na msanii Petra the rap queen.Tulipowasiliana na manager wa Undepicted film and photography alitueleza Kuwa huyu ndio mwanzo wa kazi tu na Watu watarajie. Makubwa zaidi kwa filamu,video na picha

BAIYOIYO-MNS WA HALFBOUNCY AMSHIRIKISHA SUSMILA KWA WIMBO MPYA.

Image
Ni msanii mwenye kipaji kikubwa,mwanzilishi wa kundi zima là Halfbouncy. Tunamzungumzia msanii MNS. Gwiji huyu amekuja vikali ndani ya Greenhauz production kwa ujio wake mpya kwa jina BAIYOIYO. Wimbo huo uliandaliwa na producer Noizer na msanii Susumila naye ameshikilia chorus na outro huku akitaja Mishemishe music empire. Swali ni je MNS wa half bouncy amesajiliwa na kampuni ya Susumila?Tukingojea kupata majibu tuskize wimbo baiyoiyo, kwani tayari upo mitandaoni

WASANII WAWILI WAPIGANIA KIKAO NA RAIS UHURU

Image
Ilianza na nusu saa na rais na sasa ni Mr President. Tunawazungumzia wasanii Ordinary Bingwa na Sudi boy.Msanii wa hiphop OB alitoa wimbo NUSU SAA NA RAIS mwaka uliopita ndani ya Thundersound records na ukazua hisia kali kwa mashabiki na baadhi ya watangazaji wa radio. Juzi Sudiboy naye akatoa wimbo kwa jina Mr president chini ya Sq records na unafanya vyema tayari. Swali ni je kati ya hizi nyimbo mbili ni msanii yupi amepitisha ujumbe ambao kweli hata rais mwenyewe akisikiza atataka kukutana na msanii huyo?  Na wimbo upi umepitisha ujumbe ipasavyo? Nusu saa na Rais ama Mr President?

JE NI KWELI NZUMARI AWARDS ZITAKUWA ZA GOSPEL PEKEE? N'GAMUA UKWELI HAPA!

Image
Baada ya tuzo za Nzumari zifanyikazo hapa pwani kupatwa na msukosuko na kutofanyika kwa miaka miwili mtawalia, mashabiki na washika dau wa tasnia ya muziki kanda ya Pwani walijiuliuza maswali mengi bila kupata majibu. Hivi majuzi baada ya mwanzilishi wa tuzo hizo Eve Adhiambo kuokoka na kumpokea Yesu kristo kama mwokozi wa maisha yake. Alikuja wazi wakati alipokuwa anahojiwa ndani ya Baraka fm na Dj Lenium na kusema kuwa tuzo za Nzumari zitafanyika ila wakati huu zitakuwa za gospel. Sababu kuu ya tuzo hizi kugeuzwa kuwa za gospel, Eve alidai kuwa ameamua kumtumikia Mungu na hii ndio njia moja ya kumtumukia. Binti huyu vilevile alidai kuwa bado yupo kwenye biashara za kuandaa matamasha. Juzi alikuwa na show moja ya kukata na shoka aliyomualika "malaika" si kutoka mbinguni Bali Nairobi kwa jina Corazon Kwamboka. Cha msingi ni kuwa kuna uwezekano mkubwa tuzo hizi za Nzumari gospel Awards kufanyika mwezi Aprili ndivyo alivyomalizia mwanadada Eve.

PAPAH ARUDI HORNET RECORDS KUDUMISHA HADHI YA STUDIO.

Image
Papah msanii mKali ambaye ni Produza shupavu amekuja wazi na kutangaza msimamo wake kuhusiana na kazi yake ndani ya Hornet records inayomikiwa na Mamasizo.Msanii huyo baada ya kuibwaga chini studio hii sababu ya kutoelewana na wasimamizi wa studio hii inayopatikana Mtwapa. Papah alinakili Hayà....." good news to all my fans bt bad & very sad news to all my ENEMIES. Frm mnday I'll b back to # HORNETREC MTWAPA. If u wsh to do any project with me 0723963096, # survivors inc."

MSANII WA HIPHOP HAPA PWANI ATEULIWA KUWANIA TUZO ZA MUZIKI NCHINI FRANCE!!

Image
Yaonekana mwaka umemwanzia msanii Kiwanja anayetokea Malindi vizuri sana.Punde tu baada ya kutoa wimbo wake unaozungumzia maisha ya ghetto za Afrika, msanii huyu ameteuliwa kuwania tuzo za muziki za NRJ zinazofanyika nchini France kila mwaka. Wimbo wake Africano umeteuliwa kwa kitengo cha African influential song of the year huku akishindana na wakongwe wa muziki kutoka Ghana, Nigeria, Afrika kusini na Namibia. Kiwanja aliyesajiliwa ndani ya Malindi Records anatazamiwa kusafiri nchini France hivi karibuni kwa tamasha hilo. Twamtakia kila la kheri kwenye shindano hilo.

MSANII RAPDEM YUPO NA RAUNDI HII AONYESHA FUNDAMENTALS ZAKE!!!

Image
Mlidhani Rapdem amepotea???La hasha!Yupo tena sana na ameonyesha umbile lake zuri.........bolingo!!!! Hebu tazama...  

JE LABDA HII NI ZAWADI YA NYOTA NDOGO YA VALENTINE KUTOKA KWA MPENZI WAKE WA KIZUNGU?????

Image
Valentine imefika navwapendanao kama Nyota Ndogo na mpenziwe hawajawachwa nyuma.  Nyota Ndogo kakukumbatia gari na twahisi ana raha sana(bila shaka!!!!)

MIC CHECK LYRICS BY CRAZY-K

(intro) A.T.L E.N.T Yeeah.. aha aha.. Crazy on this one! …yeah!! VERSE ONE Me ndo maziwa nipe sumu nala nashiba na sifi, Gafla nipewe bunduki naanza na marafiki, Tuzo za nyumbani mshindi anapewa jirani, Yani mziki umekua siasa ufisadi toka zamani, Wananita kisirani sababu nawababaisha, Yani miaka ikiongezeka ndo nazidi kua wiser, Nafichua siri zao cheki wanaziba nyuso, Nachozingatia ni pesa sihitaji kupewa tuzo, Huaga simple sana, na saazengine friendly, Lakini sina time na vitu hazinijengi, Sihitaji story nyingi za watu hazinifai, Ka huongei kuhusu pesa basi tuonane badae, Ikikubamba usinyamaze we piga nduru kabisa, Unajiita we ni mkali njoo nkupoteze kwa cipher, Eti ntapotea skuizi nafanya commercial, Street nasaka pesa lazima nitoke jasho, These rappers are weak ndo mana nakuja faster, Me nata waniogope napunch kwa kila stanza, Nafanya kazi hua sipendi kujisifu(ok) Minajisifu lakini so kila siku… (CHORUS) Mic check one two one two, Mic check one two one two, Mic check one two wh

Miss Tourism Mombasa 2014

Image
The MISS TOURISM FINALS are here. MOMBASA COUNTY is honoured to have Tima Keilah representing Mombasa County. Lets come together and VOTE! VOTE!VOTE! Vote Tima Keilah Miss Tourism Mombasa 2014 to be shortlisted in top 10 of the 47counties during the 2014/2015 MISS TOURISM NATIONAL COMPETITION.. Type a text mobile message "MOMBASA' and send to 20417...

"NISHAWAHI CHOMA MTU".... ...SIRI YA NYOTA NDOGO YAFICHUKA!!!!!

Image
Kumbe msanii Nyota Ndogo ni mwenye hasira kiasi hiki? Binti huyu anayevuma kwa kibao MAPANYA alinakili kuwa ashawahi choma mtu kwa moto......cha kushangaza ni kuwa ashawahi piga picha huku ameshikilia bastola.  Je Nyota ni mkali kiasi hiki???Nyota aliandika hivi.... Nyota Ndogo "Je unajua kwamba nyota ndogo ameshawai kumchoma mtu kwa moto? Kisa? Jamaa alilazwa hospitali wiki mbili . Kumbuka nilikua miaka kumi na tatu na nne hapo. huyu jamaa aliwai kuimba kitu flani kwa dadake., alipotoka ilikuaje? Ungependa kujua?"

Lovemumz arudi tena chini ya Tee hits studio

Image
Binti mshindi wa tuzo za Nzumari na Coast awards amerudi tena kwa kishindo kikuu. Mrembo Huyu ambaye yasemekana alikuwa Tanzania amerudi na kuruka ndani ya Tee hits record na kutayarisha kibao kikali kwa jina Melody. Mashabiki kuweni tayari kuupokea ujio hii mpya.

Celeb Picture of the day: Christinah Korosso

Image
Image
Alishika sana chart za muziki wa pwani na kuingia mitini. Baada ya kimya kirefu mkali wa hiphop ambaye wengi hupenda kumsifu kiupande wa commercial alirudi kimtindo na kutubwagia zigo kali kwa jina MIC-CHECK. Katika wimbo huo Crazy-K amesema wananiita kwa Cypher na bado nawashinda.....mara wanakuja wanapotea kama nyimbo za grandpa . ...Hii inadhihirisha wazi kuwa kunayealiyekuwa anamuingilia hasa kwenye sanaa ys pwani kwani pwani ndiko one hit wonders wengi.Je unadhani ni nani aliyekuwa akishambuliwa kwa diss hii?

Battle of the titans Susumila vs Escobar

Image
Leo tuangalie nani ana hits kali kati ya Susumila na Escobar.   1.Kaka Saidi vs Siasa duni 2.Bachelor boy vs Vurumisha 3.Kijana jitume vs Kaa Chonjo 4.Ngoma itambae vs Kamuti 5.Hidaya vs Hadija

SIRI ZATOBOKA!!! HIVI NDIVYO BAADHI YA WASHIKA DAU WA SANAA YA PWANI WATAKAVYO SHEHEREKEKEA VALENTINES DAY!!

Image
Ni mwezi wa mahaba na maloveydovey kemkem. Mpekuzi wetu wa umbea alipata mpenyo na kugundua baadhi ya mipango ya valentines day ya celebrities hawa wa pwani------ Hustlajay Maumau   "Valentine to me means nothing because i practice daily for my love to the nation to see it change i will look for a lonely heart in the street or nearby community and show them love. Don't celebrate your love on one day, but we should celebrate our lovers everyday" Sis Shanniez   "Nitaspend na mafans wangu Malindi" Benso   "Imagine I didn't plan anything for Valentine's" Eve Queen Adhiambo "Valentine is a special day that was set to celebrate love and definatly I will not be left aside on this year....on valentine's Eve, I will have an event,The Ciroc  all white party hosted by socialite Corazon Kwamboka and on valentines day my model boyfriend and I will be at shimo la tewa prison for my project helping the kids in prison and a

MSANII SENIOR DODGER APATA AJALI NA KUUMIA

Image
Ni habari za kusikitisha za msanii Senior Dodger aliyevuma kwa kibao 'fall in love' aliyepata ajali mbaya.Senior alipachika picha kwenye mtandao wa facebook zinazoonyesha kuumia kwake. Pwani Usanii twatuma pole zetu.

SINGA BABS AKIMSHIRIKISHA KENDI-TONITE

Image
Huku sanaa ya pwani ikizidi kupata mpenyo kwenye soko la Nairobi msanii Babs hajawachwa nyuma.Gwiji huyu chini ya usimamizi wa Re-union entertainment na studio ya Mandugu dijital amebainitumebaini kuwa anao uwezo mkuu wa kuitikisa sanaa sio ya Kenya pekee bali Afrika Mashariki.Babs kwenye ujio wake mpya amemshirikisha binti shupavu mwenye umahiri kwenye tasnia ya muziki kwa jina Kendi.Wawili hawa walijitwika jukumu la uwapa burudani na k wa pamoja wakaandaa kibao kikali kwa jina ‪#‎ tonite‬ . Unapousikiza wimbo huu hauta kuwa na budi kutikisa kichwa na kukubali utamu wake uliokolea kwani produza Scotch Fingaz aliamua kuunda mdundo wenye mvuto unaoziyeyusha hisia na kumpa msikilizaji nburudani tulivu la kukata na shoka.Basi ya nini tutumie mate ilhali wino upo? Tayari wimbo huu upo hewani kwenye vituo tofauti vya redio na umejaa mitandaoni.Utafute,usikilize burudani la kiuhakika.

"SIJAFA BALI NI ACCOUNT YANGU ILIKUWA HACKED" FLIM-C AONGEA BAADA YA WATU KUDHANI AMEFARIKI.

Image
Msanii Flim-C afufuka au tuseme hakuwa amekufa!Baada ya habari za msanii Flim-C eti amefariki,washika dau na mashabiki walianza kutuma jumbe zao za rambi rambi ila habari ni kuwa msanii huyu hajafa.Tuliwasiliana na msanii huyu na akatueleza kuwa sio yeye aliyeandika kuhusu mambo hayo bali ni mtu mwingine aliyehack account yake ya facebook na kuandika hivyo.Flim alitueleza kuwa hakuna vile anaweza kujichafulia hadhi na kutatiza familia yake kwa kusema eti amekufa.Mkali huyu wa kikosi cha Micharazo clique anayevuma kwa kibao 'tuje kule' alinena haya........ "Mimi sijafa na nipo salama salmini.Kuna jamaa amehack na kuingia kwa account yangu ya facebook.Nadhani alikua anataka kuniharia hadhi yangu.Hio picha ni yangu kweli ila sijafa.Nipo sana na nitazidi kuwapa burudani kemkem." Habari ndiyo hiyo kwa waombolezaji.Futeni machozi.