PRESENTERS WA COAST BURE KABISA......Wasanii watoboa siri ya hongo na rushwa!!!!!!


Leo hii msanii fulani alituandikia ujumbe wa simu na kukashifu vikali stesheni moja ambayo hatutaitaja jina kwa sasa. Msanii huyo alitueleza kwa hamaki kuwa stesheni fulani leo hii imempa shavu mwanawe CHAMELEONE wa Uganda ambaye hajui kuimba kabisa na wala hana kipaji. Presenta flani anayesifika hapa pwani aliicheza nyimbo ya mwanawe Chameoleone wa Uganda sana huku akiirudiarudia ilhali nyimbo yenyewe ni mbovu mwanzo hadi mwisho. Hivi ndivyo alivyotulalamikia........
"Kunao wasanii wakali underground hapa pwani wenye talanta za kuaminika ilhali hawachezwi hata mara moja, kazi yao ni kuwaitisha hongo na kuweka muziki wao kapuni. Leo hii mtu wasiyemjua wanampa shavu kwa wingi kisa na maana ni mwanawe supastar Chameleone. Je ni wasanii wangapi hapa pwani wanapewa airplay Uganda?"
Vilevile msanii huyo aliongezea kuwa mapresenta wa pwani huitisha donge nono ili kucheza muziki wa wasanii wanaoibukia

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!