Posts

Showing posts from September, 2014

DADDY SELLE,ALKENIA LUV..wazua vijimambo mambo visivyoeleweka! Soma upate uhondo!

Image
 Nakumbuka vizuri sana mwezi February mwaka huu msanii Daddy Selle alitangaza wazi kuwa amewacha muziki kabisa na ameamua kuwa mcha Mungu, msanii huyo aliyekuwa kwenye kikosi cha studio ya Mwamba records alisema kuwa amewacha mambo ya ulimwengu na anafuata kanuni na sheria za uislamu daima dawamu. Vilevile tusimsahau msanii Alkenia Luv, msanii gwiji wa RnB hapa pwani. Alkenia Luv miezi michache iliyopita aliokoka na kuahidi kuimba muziki wa injili. Jambo la kushangaza ni kuwa yuyu huyu Daddy Selle aliyedai kuwacha muziki na kumtukuza Mungu leo hii ameachia kibao kipya kwa jina NITAMUOA.Maajabu hayaishi. Mwenzake Alkenia Luv hana haya hadi leo hajawahi rekodi hata wimbo mmoja wa injili. Cha kushangaza wanaendelea kuwasifu mabinti na mapambo tu, Mungu kando!!!

MSANII WA PWANI AFUNGA BONGE LA HARUSI!!!; TAZAMA HAPA!!

 Baada ya Msanii Benso akimshirikisha Miss GG kwa wimbo PHONTO wawili hao wamerudi tena kwa kufunga harusi iliyoandaliwa video kali kwa jina I DO. Tizama hapa

NUSU SAA NA RAIS LYRICS - ODINAREH BINGWA

Yeah..Odinareh Bingwa,Skizza.. Picture me bila suti ka Easy E  ndani ya state house though najua sio easy G  pamba ni dungaree apiel nade tsho ya polo  Chini ni timba ju ngepa macho angolo  Chini ya ulinzi mkali kwa halls za white  Presidential security black suits are tight  Na napenda architect ya huku ndani big pillars  Walls zina art paintings na big pictures  Za jommo arap moi kibaki na wakoloni  Zingine za rais wetu cku zake za utotoni  Mara nafikishwa afisi ya rais kenyatta  Karibu,utanywa nini?  kahawa nyeusi ntapata? Bila shaka!! kwa ile harakati ya kufanya vijana wa stay positive, Ka damu ya poko vct!! Cctv cameras hadi kwenye sakafu  Ac hadi chooni hali ya anga barafu  mara anaingia rais mambo vipi Odinareh?  Mbona mzuka mtukufu nipe ndonga hope kaleeeh!!  [Chorus] Ningepata tu Nusu saa na rais Najua wengi wetu twatamani fursa hio rahis  Dakika salasa hivi na Orezzo Nimpe mawazo yangu ni venye sina uwezo x2  [Verse2]  Rais akadai Odinareh karibu keti, A

DONDE SAMORA SHARES SEVEN THINGS YOU DIDN'T KNOW ABOUT HIM:

Image
 Donde Samora the founder member of mashavmashav, many know him through his comic humour, deep voice and last but not least a good radio personality who still rules the airwaves upto date. Donde shared with us his little secrets........wengi wetu tulikua hatujui........ LIGHTS,CAMERA,ACTION........  1.Nilikua Mwenyekiti Wa Jumuia Ya MT.Anthony Mtopanga Estate Kanisa Katoliki La Mtopanga kwa miaka miwili.  2.Nilikua Presenter Wa Kwanza Kuresign Kazi Baraka FM Wakubwa Walipoanza Kuwatishia Wafanyikazi.  3.Mke wangu ni graduate wa Kenyatta University na anaendesha shule zake kadhaa hapa Mombasa. 4.Nilisoma Kenya poly, kenya school of monetary studies na Kenyatta University  5.Nilisomea Banking Diploma but sikuget job ya Bank ndio nikaingia mambo ya mass communication.  6.Nilikuwa Traditional Dancer Nikiwa Mukumu Boys.  7.Nina Watoi Watano. First Born Yuko Kenya High Form 1

WHAT IS HAPPENING TO PWANI TV CREATIVE TEAM CREW?

Image
We all know Pwani TV not only for it being the first and only TV Station In Coast, But also of its Extravagant Graphics and animation having being unique from any other TV stations in Kenya but for the last 3 months things have being loosing up. So i decided to go deeper and find out the source of the problem. That's when i heard of the guy known as Hetch Limz, he is among the first people when Pwani TV was brought to life. Limz was the Digital media manager at Pwani Tv. Hetch Limz is mostly known as Limz, he is an IT expert and a professional graphic designer i.e still and motion graphics. He runs his own company by the name Hetch Graphicx, check out his page https://­www.facebook.com /­­hetchgraphicx.  In his own words a good graphic designer not only knows which software to work with but how to play around with all (softwares) to achieve that creative aspect. He emphasizes that graphic designing is all about creativity and interest. From a strong source its sa

THESE ARE MY CONFESSIONS! EVE WA NZUMARI AONGELEA YOTE YANAYOMHUSU!!!

Image
Eve Queen Adhiambo mwanzilishi na mmiliki wa Nzumari awards ameamua kufunguka na kudokeza yote yanayomkumba waziwazi. Binti huyu ambaye ni mshika dau mkuu kwenye tasnia ya muziki wa pwani alinakili haya kwenye ukurasa wake wa facebook........."Hii barau na waandikia marafiki zangu wapenzi wa fb kuwaeleza mbivu na mbichi kunihusu, kwanza kabisa namshukuru Mola kwa maisha yangu na mapenzi tele alio nayo kwangu mimi, maisha ya Ustar inataka moyo tena uwe mtu usio ya sikiliza ya watu wanapo kunena vibaya, nilikuja kutana na my kaka Director#Billy Ogoda# alipokuja kunifanyia interview na baada ya hapo tulianzisha kipindi, alikua ameskia mengi kunihusu na kama wengi wenu alikua akiamini yote aliyo ya soma kwa magazeti kunihusu na chochote alicho kiskia kwa watu, baada ya kunijua kwa undani hapo basi ndo aliamini mengi yanayo andikwa na kusemwa kunihusu ni porojo, maisha ya Ustar inabidi kufanya mambo mengine ili upate kiki na uzidi kuongelewa ndo usipotee kwa midomo ama

COAST ALL DIVAS AFFAIR!! WANADADA KUMI WAHITAJIKA HARAKA KWENYE COLLABO YA SQ RECORDS!

 Chini ya produza Amz Jadidi, SQ records inawaleta pamoja wasanii chipukizi wa kike kumi kufanya collabo kali. Produza Ammz alinena haya kupitia facebook....." Je, wewe ni msanii wa kike unayechipuka kutoka hapa Msa na unahisi una uwezo wa kuthibitisha talanta yako? Jiunge na wenzako kwenye collabo kubwa ya wanadada 10 inayoendelea kufanyika. Masharti; Usiwe msajiliwa wa studio yoyote na usiwe umechezwa katika radio yoyote. Piga nambari....0789601555." Kina dada ni wakati wa kuskika,nafasi imejitokeza

WILBERFORCE WA HEARTBEAT ENTERTAINMENT ATOA ONYO KALI!!

Image
 Wilberforce Jeff Mwikya ambaye ni promota wa kusifika hapa pwani, ametoa onyo kali kwa wanaotumia jina la kampuni yake kutafuta show na kuwalaghai wasanii. Promota huyo kwa hamaki alitueleza kuwa kuna baadhi ya watu wanaowahadaa wasanii na washika dau wa wa muziki kupitia jina la kampuni yake HEARTBEAT ENTERTAINMENT. Promota huyo alinena haya......." P RESS RELEASE!Am hereby giving strong warning kwa wale wenye kujipa shavu using my own signed company HEARTBEAT ENTERTAINMENT. Mtu yeyote atakayepatikana akiwalaghai wasanii au mtu yeyote using the label without my consultation will be sued acordingly....Simba akinyeshewa haimaanishi kalala. " Habari ndio hio,washaipata!

WASANII WATANO WA PWANI WALIOSINGIZIWA KUWA ILLUMINATI: pata ukweli hapa!

Image
Huku sanaa ya pwani ikizidi kunawiri, miaka miwili, mmoja au hata miezi michache iliyopita wasanii wenye vipaji toka pwani walioinuka na kuipiku sanaa ya Afrika mashariki. Wasanii hao walisingiziwa kuwa katika kundi la waabudu shetani au ukipenda illuminati(kama wengi wanavyoliita)  Baadhi yao ni:   1.KIDIS Kidis Nesphory Simbiga au ukipenda 'The Jembe'  Alichipuka kwa kasi na kufanya remix ya wimbo wake 'kamua leo' ndani ya studio za grandpa records Nairobi. Hapo alipata umaarufu mkubwa mno na show nyingi zilifuata. Kilichotanda magazetini na mitandaoni ni kuwa Kidis yupo illuminati. Msanii huyu alipuzilia mbali madai hayo.   2.CANNIBAL  Alipojiunga na Prezzo na kutoa kibao MY CITY MY TOWN fununu ziligonga mitaani kuwa amejiunga na illuminati. Canninbal kiupande wake hakuongea lolote kuhusu madai hayo.Kimya chake kilikuwa jibu la kutosha.   3.ROJO-MO  Rojo mo japokuwa hakusemwa sana, kuna uvumi ulioenea kuwa yupo katika kundi la illuminati.

TOP TEN COASTAL KENYA SONGS: PWANI USANII MUSIC CHART:

Image
 10.NUSU SAA NA RAIS-ODINARE BINGWA(new)  9.ILINGI-SHINEY ft DAZLAH (new)   8. DOGO RICHY-HAYANA MJUZI  7.DAZLAH-BANGEREBA  6.NYOTA NDOGO & AMOURY BEYBIE-BARIDI   5.MAJID-UNGENAMBIE MAPEMA  4. JOVIAL-CHANDA CHEMA  3.HIDAYA-SUSUMILA & CHIKUZEE  2.ESCOBAR,K.ROSTO & SUDI MANJEWA-YENDE YUYE  1.SUDIBOY & AMILEENA-NAONA BADO

MEET MAYBEL: THE NEW COASTAL DIVA SENSATION.

Image
PWANI USANII: Whats your real name and your stage name? Maybel: My real name is Maybel Wendo Akinyi. I'm half Luo half kikuyu. PU:How old are you and when did you start music? Maybel:Im 17 years old and I started singing back then while I was still young attending sunday school.I started writting musoc three years ago. PU:How many songs have you recorded so far? Maybel:Four songs. Mapenzi which I was featured by fellow male artiste Reyza,Tabasamu remix which was a combination of coastal artistes and Twaayf holykraft kids,Without you which is a gospel track and a new song which i'm still working on. PU:Which producers have you woked with so far? Maybel: i've worked with producer Billy Moses of Newdawn studio who discovered me during a church concert and producer Baindo of Bigfoot production niliyetambulishwa kwake na Godwin wa Pwani Usanii. PU:What inspires you to do music and who is your role model? Maybel: The fact that God blessed me with a sweet v

KINGSTING NA BEDBUG WARUDI TENA KIMUZIKI!!!!

Image
Je mnakumbuka enzi za nyimbo ‪#‎ sonai‬ na ‪#‎ anisa‬ ? Nyimbo hizo zilizopamba moto enzi hizo mpaka sasa, zililetwa kwenu na wasanii wakali Kingsting na Bedbug. Baada ya hapo kimya kirefu kilifuata ambapo yasemekana kuwa Bedbug alikuwa amerudi kwao nchini Uganda. Kingsting kiupande wake alifungua kampuni yake ya kuandaa matamasha kwa jina TAMASHA ENTERTAINMENT, vilevile aliendelea kufanya muziki ila ni baadhi ya vibao vichache tu vi livyovuma kama kibao SHEREHE. Juzijuzi Kingsting alitoa wimbo mkali kwa jina MOMBASANI SHWARI ulioandaliwa na video director ENOS OLIK wa Nairobi.Wimbo huo ambao kwa sasa unafanya vyema katika chati tofauti za muziki ulidhihirisha kuwa Kingsting anao uwezo kipekee. Katika mahojiano hapo jana ndani ya Baraka fm Kingsting alidokeza kuwa msanii mwenzake Bedbug amerudi tena na wapo tayari kuwaangushia burudani la kukata na shoka kama zamani. " Bedbug yupo Kenya na tayari tushaanza maandalizi na mipango kabambe ya kufanya kazi pamoja

KIGOTO MMBONDE ANOGA KIMAPENZI!!

Image
Mkali wa mafleva ya RnB na afro-fusion na aliyekubalika na wengi sio mwingine bali yuleyule Kigoto Mmbonde ametangaza msimamo wake rasmi kuhusu maisha yake ya mahaba. Mshikaji huyu ametiririka hisia zake katika wimbo wake mpya NIPENDE. Kigoto ameandamwa na scandal nyingi za mahaba hivi karibuni ndiposa akaamua kujieleza kupitia muziki. "Wimbo mpya nimefanya hornet chini ya producer TK2 ngoma yaitwa nipende. Halafu vilevile mashabiki wawe tayari kwa video mpya ninayoitoa karibuni ya goma langu la ridhika," alitueleza Kigoto.

ILINGI-SHINEY NA DAZLAH WAJIBIZANA!!

Image
 Je pesa zinaweza kukupatia nini? Mali? Amani? Marafiki? Mapenzi? Umaarufu? Kukupeleka peponi? Au kuuona ufalme wa mbinguni? Haya ni maswali ambayo wasanii Shiney na Dazlah wanayajibu kupitia muziki. Katika wimbo mpya ILINGI ulioandaliwa ndani ya BIGFOOT PRODUCTION maswali haya yamepata majibu kutoka kwa Shiney na Dazlah,wawili hao wameshirikiana na kutueleza mambo yanayoletwa na pesa. Kupitia mtindo wa lingala wimbo ilingi ni wa kipekee na uliachiliwa rasmi jumapili iliyopita ndani ya pilipili fm.

SEVEN THINGS YOU DIDNT KNOW ABOUT HUSTLA-JAY.

Image
Hustla Jay shares seven things you didn't know about him.  1 2 3 lights....camera...........action.......!!  1. I'm a true hustler, i never give up.  2.I'm down to earth and simple  3.I have two personalities - i quite office work for the love of hiphop  4. I can survive anywhere i am good at making friends.  5. I love all people i'm a voice of the common man -i speak things the way they are fear nothing.  6.I was born in Mtongwe and destined for change in Mombasa music industry no matter where i go coast is my home.  7. I am halfcast of Kamba and Mijikenda (I'm from Kilifi) . . . . .with Ethiopian roots!

WASANII WA PWANI WANATUMIA NGUVU ZA UCHAWI NA UGANGA? pata ukweli hapa

Image
Ni dhahiri shahiri kuwa lisemwalo lipo na kama halipo laja. Story na visa vingi vya kurogana na kuenda kwa mganga katika sanaa ya pwani vimetambaa na kuenea mitaani. Japokuwa sio wote wanaokubaliana na kasumba hizi ni juzi ambapo msanii Majid kule kule wa jungle masters alipokuwa mgonjwa hali mahututi na lililofuata ni watu kusema kuwa karogwa na msanii mwenzake, tena rafiki yake wa karibu. Vilevile tusiwasahau Sokoro na Pharaoh watu waliongea sana kuhusu hali zao na baadhi ya wengine kudai waliendewa kwa waganga. Jana katika kipindi cha Radio kaya kinachoitwa CHIPKIZI ZA KAYA mada hii iliongelelewa kwa kina na wengi wa mashabiki wakijitokeza kuchangia. Mada yenyewe ilikuwa hivi -Uchawi, Uganga .... etc. Je ni ukweli ushirikina upo katika tasnia ya mziki pwani...? Je ni kweli katika karne hii ya 21 bado kuna baadhi ya wasanii wanaomini kutoka kimziki mpaka uende kwa babu?- Tukinukuu kutoka kwenye ukurasa wao wa facebook,baadhi ya watu walitoa maoni kama haya. David

DOGO RICHY ATETEA JUNGLE MASTERS.

Image
Msanii Dogo Richy hastahimili maneno ya watu wanaoneza chuki na malumbano kwenye kikosi chake. Msanii huyo alikuwa na haya ya kunena kupitia ukurasa wake wa facebook na......" Jungle masters is still strong managing almost 6 artistes si mchezo our big bro Emmy d amekuwa na kazi ngumu, bt we are together, what i can tel ma brothers Lypso Majid Harsh B ,Emlendy and others siku zote shetani huvamia mahali kuna mkono wa sir GOD ,we wont give up na kama wewe umekuwa fan wa jungle toka long time, big music inakam GOD bless our Team plus our C.E.O Adio sema jungle 4ever...."

PAT-C ARUDI TENA KIMUZIKI!!

Image
Alivuma kwa kibao nakuhenza kilichofanya vyem sio pwani pekee bali Kenya nzima. Tunamzungumzia msanii Pat-C. Gwiji huyo ambaye alinyamaza kiasi na kutoa vibao vingine ambavyo havikutamba sana, leo amepasua mbarika kuwa wakati umefika wa kutawala kama alivyotawala zamani. Pat ama kwa jina lingine kombe amerudi kwa kishindo na yupo na ujio mpya kabisa kwa jina NAHUMANYANE,Tulipomhoji alikuwa na haya ya kunena........."niko na nyimbo mpya inaitwa NAHUMANYANE ilitayarishwa na Crack sound by jcrack, napenda sana vile unapromote local artists"

Odinareh Bingwa amjibu Gates

Image
Iwapo umekuwa ukifuatlia story ya Odinareh Bingwa na Eric Gates, basi lazima ushafahamu kuna beef inatokota chunguni.....Hivi ndivyo Msanii huyo wa hiphop alivyomjibu Mtangazaji huyo wa Pwani FM "when 99% of the students in your university are dumb MR.LECTURER you need to change that class..hio si campus ni mental institution..same students every year kwani hawa graduate?? # DumbStudents # Id*ntKissA**

PRESENTER GATES AKASHIFU NYIMBO MPYA YA ODINAREH BINGWA LIVE ON AIR.

Image
Ni juzi tu tulipotangaza kuwa Odinareh bingwa,msanii wa hiphop hapa pwani anawachilia kibao kipya kwa jina NUSU SAA NA RAIS. Leo hii kibao hicho kilichokuwa kinatambushwa live on air kilipondwa na kukashifiwa vikali na presenta wa show ya Mashavmashav pwani fm Gates mgenge.Presenta huyu mwenye umahiri mkuu kwenye tasnia ya muzki wa pwani alidai kuwa wimbo huo Odinareh amechemsha kabisa na hasa pale anaporap kuwa Senator Mike Sonko huvuta.Hayo ni maoni ya Gates mgenge tu,je wewe yako ni yapi. 

NYOTA NDOGO ATAKA KUPIGA TIZI:ADAI KANONA!

Image
Gwiji mama mlezi wa sanaa ya pwani,msanii Nyota Ndogo amefunguka na kudai kuwa anataka kwenda gym.Msanii huyo ambaye wengi wanamfahamu kwa vibao kama; watu na viatu,mambo kombo na vingine vingine vingi alinakili kwa ukurasa wake wa facebook kuwa mafuta yamezidi mwilini na wakati wa kupiga tizi kupunguza futa hilo kabla halijazidi.Kwa sasa Nyota anavuma kwa kibao BARIDI alichoshirikiana na Amoury baybie.

EVE QUEEN AFUNGUKA KUHUSU TUZO ZA NZUMARI 2014.

Image
Huku sanaa ya pwani ikiendelea kupamba moto na kuwa kali zaidi. Wasanii wanazidi kuchipuka na waliojuu wanazidi kupanda juu zaidi, Huku wengi wakitazamia tuzo za muziki ili juhudi zao zidhihir ishwe, mwanzilishi na mkurugenzi wa NZUMARI AWARDS Eve Adhiambo aka Queen amejitokeza na kuvunja ukimya wake kuhusu tuzo za mwaka huu. Tuliwasiliana naye na alikuwa na haya ya kunena.' "Kila kitu namuachia Mungu, nimegundua kuongea mipangilio ya kazi kabla ufanikishe uingiwa na midomo mibaya na wenye wivu, kwa sasa sitaki kuongelea Nzumari, niko busy na shooting ya Ubishoo: ya pwani tv, ila tumuombe Mungu na yote yawezekana kwa mapenzi yake........"

KUTANA NA MR.KATSOPOLE MSANII CHIPUKIZI

Image
WANAKUITAJE MAJINA KAMILI: La serikali ni Kevin Mwarua Hassan na la usanii mr katsopole.  TUELEZEE JINSI ULIVYOANZA MUZIKI:  Mimi nimeanza kuimba toka darasala tano nikiwa kilifi primary nilipenda sana mziki wa matonya nilikuwa kila mara mimi na mziki.  MUZIKI UPI WA MSANII ULIKUVUTIA ZAIDI ? msaani niliyemuona kwamba ana sauti na nilianza kupenda mziki wake si mwengine ila chikuzee napenda niwe kama yeye.  NA JE ULIANZA LINI KUREKODI? niliendelea hadi nami kuingia lango la kurekodi nilirekodi song yangu ya kwanza iliyoitwa neema wengi waliipenda wengine wakichukia ndipo nikajiita mr katspole nilipenda sana song zangu . TUELEZEE KUHUSU WIMBO WAKO MPYA NAMALA NIGUTE ULIVYOPATA UMAARUFU: Wimbo wangu namala nigute nilikuwa mtaani nikitembea nilikuta road show ya pilipili FM niliimba song mmoja wakasema niwape song zangu zotenashukuru Mungu kwa yote.