MSANII ANAYECHIPUKA AANGUKIA BONGA LA DILI LA KINYWAJI CHA EIGHT VODKA!!!
MSANII ANAYECHIPUKA AANGUKIA BONGA LA DILI NA KINYWAJI CHA EIGHT VODKA!!! Yaonekana mwaka umemuanzia vyema msanii Nassizu Murume. Msanii huyu aliyesajiliwa na kampuni ya Watanashati Classic ameangukia bonge la dili itakayo mpa yeye kiki ya kueleweka kwenye ukumbi wa burudani. Nassizu,kwa sasa ndiye brand ambassador wa kinywaji cha pombe ya eight Vodka kampuni ikiwa ya Tihan limited company. Huku akisubiria kuachia video yake mpya iliyoandaliwa na Johnson Kyalo,msanii huyu vilevile yupo katika pilka pilka za kupiga show kalikali nje ya nchi. Mwaka Jana ,Nassizu Murume aliachia kibao MAWAZO kilichopeta sana na kumpa jina la kisawasawa.