PRODUZA KHALID:"Nitajie msanii yoyote aliye hit nikwambie presenter gani anamu manage na kina nani wamembeba..."

Tukinukuu moja kwa moja kutoka kwa account ya Khalid Produza wa A Million records akizungumzia kuhusiana na branding......

#Branding
Neno 'Branding' limekuwa likitumika vibaya na watu wengi sana, sanasana watu wa media. Neno hili linatumika kudhalilisha, kunyanyasa, kudhulumu wasanii bila kujua.

Wanaotumia neno hili huwa Wana nia fiche ya kukuweka kapuni bila ya wewe kulalama ili uwape nafasi wawabebe wanaotaka kuwabeba.Ukweli ni kuwa in Africa hakuna msanii aliyeweza kutoka au ku hit kisa na maana ameji 'brand'. 90% ya wasanii walio hit wamebebwa na media au watu fulani maarufu. Na huu ndio ukweli wa mambo.

Nipe majina ya wasanii watano unaodhani walijibrand ndio wakahit nami nikwambie ni nani amewabeba bila ya wewe kujua ndio Waka hit. Ukweli ni kuwa presenters wengi ni managers wa wasanii japo hili huwa linafanyika chini ya maji. Kinachofuata ni nyimbo kuchezwa kila siku na shows kupewa hao ili wapate commission.

Kuna tofauti ya msanii kuwa na pesa na kufanya branding. Wengi hudhani kuvaa vizuri, kuwa na gari, ku floss ndio branding. Ukweli ni kuwa hakuna msanii alizaliwa tajiri, na wote ukiona TBT zao utacheka jinsi walivyojikondea. Lakini baada ya kubebwa, wakapata shows na sasa Wana pesa, kwa hivyo kuvaa vizuri, ku floss, kufanya video za mamilioni sio shida. Mbona kama kweli ni branding, mbona hawakufanya video za mamilioni walipoanza, waliishia kufanya video za kijijini na uswahilini ndio kukwepa gharama.? Iweje msanii anayeanza sasa utarajie mamilioni? Atapata wapi hiyo hela?

Msanii Mpendwa unaejituma, mtu asikwambie ujinga wa branding, wanawabeba wanaotaka kuwabeba na watawawekea vikwazo wasiowataka. Akothee kufikia sasa ametumia zaidi ya 30 Million kufanya branding, mbona hapewi show akalipwa 2 Million na ukweli ni kuwa anastahili? Wacha 2 Million, hata 100k hatapewa kwa sababu hataitwa..... Halafu mtu akwambie 'Branding', Mwambie kidole cha kati.....

Nitajie msanii yoyote aliye hit nikwambie presenter gani anamu manage na kina nani wamembeba.....

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!