PRESENTA ASINYA WASIKILIZAJI KWA PROMO ZAKE ZA KUUZA T.SHIRT LIVE ON AIR!!!


Huku show za redio zikiendelea kupamba moto kila uchao kwa kutifuana kivumbi kwa ustadi wao wa sampuli za muziki,matangazo na interviews motomoto. Eneo la pwani halijaachwa nyuma kwani show zao zina ushindani mkuu hasa zile zinazocheza muziki wa kizazi kipya. Hii imeleta hisia tofauti na maoni ya mashabiki wa tasnia ya muziki wa pwani. Shabiki mmoja alionekana kugadhabishwa na presenta fulani mwenye tabia ya kufanya biashara ya kuuza t.shirt live on air. Presenta huyo mwenye umahiri mkuu hapa pwani yasemekana ana majivuno sana na badala ya kuwapa wasanii promo ya kuuza cd zao anafanya biashara zake binafsi. Tukibana jina lake,bingwa huyo ana tabia ya kutembea tembea na kuwabeba wasanii kwa kila show anayoalikwa na kupanda jukwaani nao. Shabiki huyo alisema hivi............"Fanya promo mashabiki wanunue CD za wasanii usifanye promo watu wanunue ma t-shirt.................."

Ujumbe ndio huo

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!