MSANII WA LIKONI APEWA KICHAPO CHA MBWA KWA KUIBA!!!


Ni msanii anayetokea papa hapa Likoni na alirekodi muziki wake ndani ya Flash records. Msanii huyo anayejulikana na wengi kama MZEE MKALI alipewa mob justice na watu baada ya kutoweka na mali za wenyewe(hatukuambiwa ni nini ila yashukiwa ni simu). Aliyewasiliana nasi alituarifu kuwa msanii huyo ambaye wengi walimsifu kwa kipaji chake alipatwa maeneo ya kona ya zamani na umati ukamvamia na kumshambulia vikali.Japokuwa alivuja na kutiririka damu,watu waliendelea kumuadhibu vilivyo. Gwiji huyo alikuwa ameoa maeneo ya Mtongwe na alijifanya sharobaro sana hata kutungiwa jina LOVERBOY. Yasemekana kuwa msanii huyo alijiingiza kwenye utumizi wa mihadarati,uvutaji bangi,mugooka bila kusahau ugoro na uraibu mwingine.
Je washika dau wa pwani,hapo ndipo usanii wa pwani utatufikisha????

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!