INTRODUCING DAVY GZE.


Pwani Usanii: majina yako kamili?
Davy Gze:majina yangu kamili ni David Haron Baraza mtoto wa mwisho katika familia yangu
Pwani Usanii:watokea upande gani
Davy Gze:naishi likoni
Pwani Usanii:ulianza mziki lini?
Davy Gze:nilianza mziki mwaka wa 2007 nikiwa shuleni japo nilikua sijarekodi.
Pwani Usanii:ulirekodi lini.?
Davy Gze:mwaka wa 2008 ndipo mwalimu mmoja aliridhika na nyimbo zangu nakuamua kunipeleka studio kurecord Flash Records ambapo nilifanya nyimbo yangu ya kwanza iliyowapa motisha watu kutaka kuskia nyimbo ya pili ila ilikua ngumu kama rasta bila msokoto kwani nilikua nasoma.
Pwani Usanii: Je baada ya kumaliza masomo. ?
Davy Gze:nilipomalza shule ndipo nilirudi kufanya kibao chini ya produza Nicky Wizzoh katika studio ya Wizzoh classic empire ambapo nilimshirikisha Sticky wa manabii tukafanya nyimbo kwa jina Siku Yangu
Pwani Usanii:ulikarishwa vipi baada ya kutulia kwa muda?
Davy Gze:nashukuru kwa wote wanaosupport kazi zangu akiwemo Kassim Mbui wa Pilipili FM pia na washikadau wa mziki pamoja na mashabiki wangu.
Pwani Usanii: Una lipi la kuambia mashabiki wako?
Davy Gze:mashabiki wangu wanipe support nami nawaahidi kazi nzuri.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!