MSWAZI MASAUTI KUMBE KASAJILIWA NAIROBI TENA!!!!!

MSWAZI MASAUTI KUMBE KASAJILIWA NAIROBI TENA!!!!!

Msanii wa miondoko ya swahili RnB Mswazi Masauti amezuka tena baada ya kimya Kirefu. Meza yetu ya habari imebaini kuwa jamaa huyu baada ya kuwachana na Lebo ya Swarnb alipokuwa amesajiliwa chini Ya produza Ted Josiah, Mswazi amesajiliwa chini ya studio zilizoko Nairobi.

Kwa mara nyingine tena,msanii huyu wa kibao cha 'Mahabuba' ameweka guu lake ndani ya jiji kuu la Nairobi na kupata fursa ya kufanya kazi chini Ya usajili wa Melwood studio ambapo atafanya kazi Na produza anayebobea, Motiff.
Produza huyu amefanya kazi na wasanii kama Khaligraph Jones, The Kansoul na wengineo.
Baada ya mawasiliano na msanii huyu, Masauti alidokeza kuwa kuna ngoma nyingi tu ambazo amefanya na hivi karibuni zitawachiliwa rasmi.

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!