UKWELI USEMWE!!NI KENYA MUSIC INDUSTRY HAKUNA CHA COAST MUSIC INDUSTRY.


Lawama lazima ndiposa tumejitwika mzigo wa kuwaletea habari zitakazowaudhi wengi ila ndio ukweli tu.Mpende msipende.Mtake msitake.Jambo moja linaloregesha sanaa ya pwani nyuma ni kujitenga na kutaka kujenga 'coast showbiz'.Hakuna kitu kama coast music industry na kama tutazidi kujitenga tuseme kunayo basi daima tutazidi kuumia na wasanii wetu kudhalilishwa kila wakati.Jina mufti na la haki kabisa ni Kenya Entertainment industry. Kwa mfano msanii wa pwani apate nafasi kuzuru nchi ya ng'ambo kwa tamasha.Atasema ametoka wapi?Kando na hilo msanii kuchezwa kwa redio za hapa pwani hasikiki Kenya nzima.Kwa hivyo anapojiskia hewani asione amefaulu,bado kazi ipo ya kuzuru pande nyingine za nchi kusambaza muziki wako.
Tulijaribu kupata maoni kutoka kwa Al-Manuel Ntoyai ambaye ni entertainment editor wa People Daily na alituunga mkono vilivyo



"I have had little time to sample the alleged "Coast Music". I fell in love with it. What some of you guys are doing is really great. Great to be on not just national platforms, but also regional and even world wide. Your showbiz is well organised to rival the multi million industry in River Road. Who knows? But time is up on this Coast music this, coast showbiz that. Why not talk about Kenyan music? Ever heard of Abuja music? NEVER. Its Nigerian Music or West African Music. Time is up. As an industry, we need to move as one unit. Not different groups. That's all"

 
Haya ni maoni yetu na yake.Itakuwa vyema zaidi kama nyie washika dau,wanaharakati na mashabiki mnetoa maoni yenu kuhusu mada hii

Comments

Popular posts from this blog

MSANII KIJANA RANNY WA KADEM KUMBE KAJIUNGA NA KIKOSI CHA POLISI........pata uhondo hapa.

MKISEMA WAREMBO HAWAJAZAWA....TAZAMENI PICHA ZA VIDEO HII INAYOKUJA!!!