Posts

Showing posts from January, 2015

TAFSIRI YA WASANII KUMI WA PWANI WATAKAOFANYA VIZURI ZAIDI MWAKA HUU.

Image
10.Ziky wa Ziky   Ni msanii mchanga aliyesajiliwa ndani ya Jungle Masters chini ya produza mkali Emmy Dee . Ziky wa Ziky amethibitisha uwezo mkali kwa wimbo wake wa kwanza na kuichukua style ya wanamuziki wa Jungle Masterz vilivyo, kama vile Dogo Richy, Majid na Lypso . Tarajieni makubwa kutoka kwa Ziky wa Ziky. 9.SHEMBWANA MASAUTY   Msanii huyu alidhihirisha uwezo wake kwa wimbo 'uko mbali' ambao japo haukuvuma sana hivyo ulimleta karibu na mashabiki zake. Baada ya hapo chini ya Liwazo records ,Shembwana alirudi kwa kibao cha dancehall 'siwezi' kilichomtambulisha Kenya nzima na kumvutia mashabiki chungu nzima. Mwaka huu, twahisi Shembwana atakuwa moto wa kuotea mbali na twatarajia burudani la kukata na shoka kutoka kwake. 8.KIWANJA   Ni dhahiri shahiri kuwa Malindi kuna vipaji na bila shaka tunamzungumzia msanii Kiwanja. Rapper huyu chini ya Malindi records amezuka vikali kwa vibao vyake ' Afrikano ' na collabo kali kwa jina 'bo

SHAME, SQ RECORDS CEO STEVE OTIENO ARRESTED AFTER HE WAS FOUND WITH AKOTHE'S STOLEN PROPERTY!

Image
SQ records CEO got the shock of his lifetime after police stormed into his house and had him arrested over theft allegations. Credible information reaching us confirms that the equipment, Akothee's sound cards and recording property were found at the scene of arrest. Akothee who together with Backstreet had gone to confirm this accompanied with Mtwapa police officers were shocked to the core since they trusted Steve to be a man of morals. This however turned out to be a whole different story and Steve had to find his way into mentioning his accomplice. According to information reaching us, Steve threw the burden to Coastal artist Brown Mauzo saying he bought them from him. Mombasa city has also confirmed that Steve had begged Brown to also make away with Akothee's Canon Camera and other studio equipment which the artist used. The police were shocked with the incident and Akothee has also confirmed the equipment were legally hers and was shocked as why such b

PATA KUMFAHAMU MTANGAAJI GWIJI 'ATHMAN AYUB MATUMBO' BABA MLEZI WA SANAA YA PWANI AKIELEZEA SAFARI YAKE KWENYE JUMBA LA UTANGAZAJI.

Image
(Akielezea mwenyewe) Nilimaliza elimu ya msingi 1993, pale Dabaso primary school, Watamu. Nilifanikiwa kuibuka mwanafunzi bora mwaka huo katika eneo lote la Gede na nikapata nafasi ya kujiunga na shule ya upili Godoma Boys. Kutokana na hali ngumu ya maisha fedha ilikuwa shida nilishindwa kuendelea na masomo Ya upili Godoma na nikahamia nchi Jirani ya Tanzania ambako nilibahatika kuendelea na masomo yangu hadi kidato cha sita pale islamic seminary school ya ununio boys. Lakini Kila jambo lina sababu yake baada ya kuhamia bongo ,miaka hio ndio muziki wa bongo flava ulikuwa inazaliwa.Kipindi hicho mziki huo ukiwa unaitwa BONGO ZANIA.Niliweza kushuhudia mwanzo wa mziki huu wakati huo wahasisi wakiwa ni kina Swaleh Jabri, Nigga One, Kyadaman, Ras Pompidu. Ndipo wakaja kina Too Proud a.k.a Mr TWO au Suguu Nigga Jay kwa sasa Profesa Jay. Nami sikuachwa nyuma kwani nilikuwa ni mwanamziki wa kufoka foka, hip hop artist Japo sikuwahi kurekodi. Baadhi ya wanamuziki a

MEET: DANIEL OKORIR A MASTER OF LIVE MUSIC AND AFRICAN INSTRUMENTALS.

Image
Daniel Okiror had barely started on his journey of creating a unique & true Ugandan genre by fusing roots instruments especially Akogo, Adungu, Adeudeu, Edodoi, Arigirigi, & African drums/percussion with modern/western instruments, mainly acoustic and base guitar, saxophone & Keys when he took a radical global minded step of pursuing his vision beyond the boarders, resulting to him becoming a Mombasa Kenya resident. Originally from Eastern Uganda, Daniel Okiror's musical roots can be traced back to the age of 3, when he first made a song called Papa Ijaka (Father...who will help me). From then on it was clear that his musical journey was going to be influenced by his experiences growing up as an orphan and indeed, this painful experience soon found an outlet in music and a strong desire to give back to the community. This makes him a unique kind of musician who uses his talent, time and resources to help African street children find a hopeful future! H

MAJID KULEKULE REVEALS SEVEN SECRETS YOU DIDN'T KNOW ABOUT HIM!

Image
Majid aka Kule Kule ni msanii aliyevuma kwa vibao vingi tu vikali vikali vikiwemo Hali,Sinyora,serebuka,Ungenambia na vinginevyo.Mkali huyu wa flavour za swahili rnb alishare na sisi siri saba zake tusizozijua---- 1.Majid hupenda kupika. 2.Majid hapendi uzururaji ovyo bali hupenda kutulia home. 3.Hapendi kuskiza muziki kwa sauti kubwa sipendi. 4.Majid hupenda sana kuskiza stesheni ya BBC 5.Hupenda kula wali sana(na hanoni!). 6.Majid hupenda kupanda maua. 7.Hupenda kupanga rangi.

KWA MARA YA KWANZA WIMBO WA HIPHOP WENYE LIVE GUITAR YA GENERAL DEFAO!!

Image
Huku sanaa ya muziki ikizidi kupanuka na wanamuziki kuwa na mitindo tofauti tofauti.Msanii wa hiphop Hustla-Jay hajawachwa nyuma.Jamaa huyu ambaye ametamba kwa vibao kama minyororo ya haki,continental scar na nyinginezo amezuka upya na kuwachia ujio mpya.Hustla ametoa wimbo ambao ulipigiwa live guitar na Onyango Onyi aliyekuwa mpigaji guitar wa muimbaji lingala mashuhuri General Defao.Pata kuusikia wimbo wenyewe hapa--------- https://soundcloud.com/hustlajaymaumau/siku-mbisha-hustlajay-ft-hakim-ziya

KIPINDI CHA ALMASI K24 CHAKARIBIA MWISHO.

Image
Twashuku tamati imefikia kwa kipindi cha kusisimua ALMASI kinachotia fora kwenye televisheni zetu kila siku.Kipindi hiki kilichojaa talanta za waigizaji wa pwani kimepewa sifa za ndovu kumla mwanawe ila kilicho na mwanzo bila shaka hakina budi kufikia mwisho.Hivi ndivyo alivyonakili MJ muiizaji machachari wa kipindi hicho................"Mr Mj aka Baba Chocha aka Mambo madogo.Jana ndio ilikuwa siku ya mwisho ya kushoot Almasi.Kumekuwana pandashuka za hapa na pale ila nimejitahidi kuwaridhisha mafans wangu kwa kufunga kazi ipaswavyo.Respect to Ashiner picture, Almasi artist,crew na mafans wangu wote ni kwa support yao ndio imenifikisha hapa nimefika.God bless you all....Nionyeshe upendo kwa kutoa hisia zako kuhusu Mj.

THE LOST RING- MOVIE

Manufaa yameenza kujitokeza jijini Malindi City,Yaani Jiji lenye mvuto wakivyake,Jiji la Utalii na Bango.Wana MARIMBA wameachilia filamu yao mpya hivi leo iliyokua ikingojewa na wengi kwa hamu na ghamu,filamu hii inafahamika kama THE LOST RING. Filamu hii imebobea mastar na gwiji wengi kama vile, Jituzee wa GBT,Marvelous, Mbuyu wa TABAKA, PrincessR, Ali Gereza na wengine wengi.shukrani Malindi Superstars.

TAMADUNI NA MILA:MSANII WA HIPHOP AFANYIWA TAMBIKO NA WAZEE.

Image
Alipotoka Uganda kwa project yake ya 'back to the source', Hustla Jay msanii wa hiphop alipotea kidogo huku watu hawakujua amepotelea wapi. Kumbe huo muda wote Hustla-Jay alikuwa ameingia umasaini kuandaa project nyingine at the same time akifanyiwa tambiko na wazee wa kimaasai. Baada ya tambiko na wazee wa kimaasai, Hustla-Jay alichukuliwa kwa familia ya Mzee Sankale. Msanii huyo aligeuzwa jina na kupewa jina linaloandamana sambamba na tamaduni za kimaasi na sasa anaitwa Ole Sankale.

KIWANJA AZIDI KUTAMBA VIWANJANI:AKIWAKILISHA 'CHOCOLATE CITY' MALINDI

Image
 Kiwanja ni msanii na producer kutoka Malindi aliyesajiliwa na label ya Malindi Records kama msanii wa mziki.Msanii huyu aliye na ujuzi wa kuunda muziki na kufoka yupo chini ya mbawa zake meneja John Okoth. Kiwanja ameshirikiana na wasanii wenzake mjini Malindi ukipenda chocolate city kwa kutengeneza muziki unaosifu mji Malindi na Mitaa yake.Kiwanja ni mmoja wa Legco tano,kikundi cha hiphop kilicho jikuza malindi city na kutoa vibao kama"Upishi bado" waliomshirikisha Susumila.Vilevile msanii huyu alikuwa kwenye collabo kali sana kwa jina '8onde chafu' akishirikiana na Marvin Brudaz na wasanii wengine.Kwa sasa video yake ya 'Africano' inayozungumzia maisha ya ghetto barani Afrika yalivyo.

PRODUZA PETROOZ AWACHA KUANDAA MUZIKI!!"

Image
Produza Petrooz ambaye ni gwiji kwenye tasnia ya sanaa ya pwani amewacha kazi yake.Produza huyu aliyekuwa Stantmastaz na kuwaandalia wasanii wengi muziki kama vile Benso,Ohms law,Dogo Richie,Miss GG,Lavichunare na wengine wengi aliamua kuingia mitini kwa muda ili aongeze ujuzi wake.Petrooz alianza kuandaa muziki tangu alipokuwa sekondari na miaka kumi na nne.Tulipowasiliana naye Petrooz alitueleza hivi............ "Sababu ni kuwa ni ko kisomo sahii. Sound engineering and am studying music that is theory so i wont have much time. But i will be back, remember i have been in this game for 7 years now and music zenye wengi twafanya hazina formular twafanya tu tupate pesa but this time i just wanna do real and good music once i come back."Japokuwa Petrooz hakutuelezea atakaa nje kwa muda gani. ‪#‎ TeamPwaniUsanii‬ twamtakia kila la kheri mpaka atakapop rudi tena kwa game.La mwisho alitueleza hivi.........."good music takes time to be ready thats why they

TEACHER DONDE SAMORA FOR EDUCATION!!! KUMBE MTANGAZAJI DONDE SAMORA MWALIMU???

Image
Ni mtangazaji wa pilipili fm,mlezi wa vipaji,mcheshi,muigizaji na hivi sasa ni mwalimu ukipenda waeza muita kwa jina lake mpya TEACHER DONDE.Mtangazaji huyu mwenye tajriba kuu kwenye tasnia ya sanaa ya pwani tulimpata maeneo ya Junda akifundisha wanafunzi.Donde alionekana mchangamfu na mwenye furaha sana huku wanafunzi wake wakishangilia na kujibu maswali kwelikweli.Tulitengeza kikao ili tuweze kuj ua zaidi kuhusu teacher Donde na alitueleza hivi........Kwanza napenda sana watoto na elimu.Shule hii ninyofundisha inaitwa Junda Bright Academy. Nafundisha Science,English,Soci­al Studies,Kiswahili na Hesabu.Class 4 na 5.Huwa ni furaha sana pale tunapokuwa darasani.Masaa yangu ya kufundisha huwa sanasana ni jioni.Mke wangu pia ni director na ni mwalimu papa hapa Junda Bright Academy.Kitu watu hawafahamu ni kuwa nilisomea Education chuo kikuu." Tulimuuliza Donde Samora vile yeye ni mcheshi na anapenda mzaha je wanafunzi humskiza kweli ama ni kumchezea h

UKWELI USEMWE!!NI KENYA MUSIC INDUSTRY HAKUNA CHA COAST MUSIC INDUSTRY.

Image
Lawama lazima ndiposa tumejitwika mzigo wa kuwaletea habari zitakazowaudhi wengi ila ndio ukweli tu.Mpende msipende.Mtake msitake.Jambo moja linaloregesha sanaa ya pwani nyuma ni kujitenga na kutaka kujenga 'coast showbiz'.Hakuna kitu kama coast music industry na kama tutazidi kujitenga tuseme kunayo basi daima tutazidi kuumia na wasanii wetu kudhalilishwa kila wakati.Jina mufti na la haki kabisa ni Kenya Entertainment industry. Kwa mfano msanii wa pwani apate nafasi kuzuru nchi ya ng'ambo kwa tamasha.Atasema ametoka wapi?Kando na hilo msanii kuchezwa kwa redio za hapa pwani hasikiki Kenya nzima.Kwa hivyo anapojiskia hewani asione amefaulu,bado kazi ipo ya kuzuru pande nyingine za nchi kusambaza muziki wako. Tulijaribu kupata maoni kutoka kwa Al-Manuel Ntoyai ambaye ni entertainment editor wa People Daily na alituunga mkono vilivyo "I have had little time to sample the alleged "Coast Music". I fell in love with it. What some of you guys are

SALAAALEE!!!TAZAMENI MITINDO YA NYWELE YA BAADHI YA WASHIKA DAU PWANI!!

Image
Dazlah Eric Gates Hypemaster Kavalier Johnny Skani Kiddis Kigoto MC Muscat Moreno Ohms Law Montana

COAST KENYA MUSIC: UNITED WE STAND DIVIDED WE FALL!!

Image
Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu huo ndio ujumbe wa mwanaharakati shupavu wa muziki wa pwani Lizz Jahsolja.Huku tukimuunga mkono (na mguu!) sanaa ya muziki wa pwani ina umoja wa ajabu.Presenters wako mbio kuwaenua wanaochipuka,waliojuu nao wanashikamana kuzidi kupenya kwenye nyanja mpya za sanaa.Bila kumaliza MUTSWANO tunanakili aliyolonga Lizz Jahsolja............. "I dont think coast industry luck unity..if your in the same boat and the boat is sinking,are you going to cuddle each and wait for it to sink or you will find a way of saving it from not sinking?!Any coast artist that is doing his or her own way doesnt mean that he/she doenst like his/her fellow artists coz if he/she succeed in the game name wont charge itabaki yeah msanii wa coast and people will start digging dip about coast artist to know more about them and to know where the hidden talent are..you can give support any how but at the end of the day we dint fight what is always on our way...Coas

JE WAMFAHAMU KASSIM MBUI??? MTANGAZAJI WA PILIPILI FM ALIYEJITOLEA KUWASAIDIA CHIPUKIZI

Image
Kipindi chake cha MisheMishe za maisha PILIPILI FM kila jumapili usiku kimesaidia na kutambulisha vipaji vingi hasa vya sanaa hapa pwani. Ndiposa hatukuwa na budi kumtafuta ili atueleze safari yake ya kuenua vipaji ilianza wapi,vipi na imefikia wapi. Kassim Mbui aeleza......... Nafahamika kwa jina kama Kassim Mbui.Mzaliwa wa hapa pwani,kwa sasa nina umri wa miaka 23 mwaka huu Inshallah nitagonga 24.Kitaaluma mimi ni mwanahabari nimesoma na nikahitumu pale TUM(Technical University of Mombasa) mwaka wa 2013 baada ya kumaliza kidato cha nne mwaka wa 2009 katika shule ninayoienzi kwa sana St Georges High school.Kazi ninayoifanya kwa sasa sio kwamba nakosea njia ila ni kitu nilichikuwa nacho nikiwa na umri mdogo sana.Wakati huo nikiskia watu kama kina George Biff Mkuzi,Omar Mwagao,Papah Mukulu,Donde Samora na wengineo.Nilitamani sana angalau pia mimi siku moja niwe naeza nikasikizwa kama hivyo. Passion yangu ya kutaka kuzungumzia maswala ya jamii itimie.Kwa sasa nina furaha

DAZLAH AMSHIRIKISHA CHIKUZEE 'KALEKALE'

Image
Yaonekana Chikuzee ndiye mfalme wa Collabo miaka hii ya sasa. Baada ya kushirikishwa kwenye nyimbo zinazokita kwenye chati za muziki kama vile Ngoma itambae na Hidaya za Susumila,Makissy akiwa na Busy'K,mapenzi nayajua yake na Chege wa Bongo.Dazla naye ameamua kufuata mkondo na kumshirikisha Chikuzee kwenye ujio wake mpya kwa jina 'kalekale.' Chini ya meneja wake Tee,Dazla amejaribu kuchanganya sauti yake na Chikuzee kuwaletea mashabiki wa pwani wimbo uliokolea fleva za pwani.Tegea wimbo huu wakati wowote kwa sasa.

MWASEMA WASANII WA PWANI MSOTO??? TAZAMA HAPA UONE WALICHOFANYA WASANII HAWA!!

Image
Amkeni kumekucha! Wakati watu wanapiga domo na wasanii kujilalamikia kwamba muziki pwani hauna mapato wasanii Nyota Ndogo na Kidis ukipenda 'the jembe' wanaringa kwa pato kuu wanalovuna kimuziki. Nyota Ndogo alidokeza kuwa kuanzia show za mwaka jana mwezi wa Oktoba amejikwachulia mkwanja kiasi cha kununua shamba. Dada huyu anayevuma kwa kibao 'mapanya' aliweka picha yake ya shamba alilonunua kwenye mtandao wa twitter. Nyota alilonga haya,"Baada ya kufanya show kuanzia mwezi wa october na december.nimeweza kununua land hii jana.am happy.mziki unalipa." Naye Kidis amefungua duka la kuuza nguo. Bila shaka muziki ukikukubali unalipa

VIDEO MPYA YA MSANII KIWANJA ITAKAYOWAZUZUA WENGI KWA UJUMBE ATAKAOPITISHA AFRICA NZIMA!!!

Image
Mwaka mpya umeanza kwa kishindo kikuu kwa tasnia ya muziki si wa pwani pekee bali Afrika mashariki kwa jumla.Kutoka Malindi mkali wa miondoko ya hiphop msanii Kiwanja atawapeleka Afrika nzima ili awaonyesha jinsi maisha ya ghetto yalivyo.Video ya Kiwanja imendaliwa kwa mtindo wa kipekee huku ikionyesha uzuri wa maisha ya ghetto yalivyo.Kwa hali ya juu,Kiwanja amejaribu kuleta hisia za kimuziki na kuzichanganya na maisha ya undani ya kijana wa kiafrika.Tayarivideo hii imeanza kupata umaarufu na imetikisa runinga tofauti hapa Kenya.Tulipata kumuuliza meneja wake John Okoth kuhusiana na video hii na alituambia haya.........."Fewer people have little experience of what the ghetto environment is like: you hear about it or vaguely see it on TV. What this video brings to it is a different perspective on what that environment is like through the eyes of an artist, Kiwanja. Our intention is to make the audience have a rush of experiences that is unpredictable and by turns st

JE VIDEO 'AIREE' YA KIGOTO IMEZUILIWA KUTOKA NA SUSUMILA??? PATA UKWELI HAPA............

Image
Baada ya habari kuchipuka kuwa video "Airee" ya msanii Kigoto imezuiliwa na msanii Susumila na Tk2 kutoka, meza yetu ya habari iliwasiliana na produza Tk2 kutaka kujua ukweli wa fununu hizi. TK2 alitueleza kuwa ni kweli kuwa msanii Susumila amezuilia video hiyo ila hajui zaidi ya hapo.Video hio iliyoandaliwa na mtayarishaji video Ricky Becko mwaka uliopita ilisubiriwa na mashabiki kwa shauku kuu kwani ndiyo ya Kigoto ya kwanza.Juhudi zetu za kumtafuta Kigoto ziliambulia patupu.

HUSTLA-JAY APELEKA MZUNGU WAKE WA KIKE KUONA WAZAZI!!

Image
Ukiona vyaelea bila shaka vimeundwa,baada ya CLD, NYOTA NDOGO, SUZUKI, KIDIS, AMOURY BEYBIE na wasanii wengine kujikwachulia wazungu hiphop heavyweight Hustla-Jay hajawachwa nyuma.  Rapper huyu anayependa kupigania haki kupitia muziki wake alijishindia mpenzi wa kizungu ambapo yasemekana alimpeleka hadi nyumbani kuona wazazi. Huku video yake ya intercontinental scar ikiendelea kupata umaarufu,Hustla-J amekolea kwenye mahaba ya kizungu na twasubiri kuona yatakayojiri.....

HIPHOP HEAVYWEIGHT HUSTLA-JAY AWASHIRIKISHA WASANII WATOTO KWA WIMBO WAKUTUKUZA WANAWAKE.

Image
Baada ya kutoa video 'Intercontinental scar' msanii Hustla-j aliyesajiliwa ndani ya S3 studios Nairobi amezuka upya. Hustla-Jay alipangiwa project hii na msanii Babaluku na kukutanishwa na wasanii hawa wachanga ili aweze kuwashirikiana nao. Wasanii hawa wadogo wanaotoka nchi jirani ya Uganda wakiwa na Babaluku na Hustla-Jay wamelenga mada inayopuziliwa sana na wasanii. Ushirikiano huu umem pa mwanamke wa kiAfrika kipao mbele huku mila na tamaduni zikiwadhalilisha.  Wimbo wenyewe unaitwa 'Amandla' {power to the women} Hustla-Jay akiwashirikisha Babaluku toka Uganda,Mc flower aliye na umri wa miaka 13 kutoka Uganda na Khamara Ashnan poet 16 kutoka Uganda. Project hii iliandaliwa na Gwiji wa miondoko ya hiphop anayetokea Uganda,Babaluku. Project hii ilyofanywa nchini Uganda iliangazia vipaji kwa vijana hasa kandanda,ushairi na muziki.Tayari video ya wimbo huu ipo kwenye maandalizi.