Posts

Showing posts from May, 2018

BEKA THE BOY AMCHAMBA OTILE BROWN?!!! NANI KAKOPI MWENZAKE??????

Image
Msanii anayebobea kwa sasa Beka the Boy amefunguka vikali na kutoa kauli yake kuhusiana na msanii mwenzake Otile Brown. Hii ni baada ya tetesi ya kuigiziana kimawazo na kifikira za kisanii. Beka,anayetokea Malindi ila kwa sasa yupo jijini Nairobi kusukuma kazi zake kimuziki, kupitia jarida La Trendin,gazeti La Pd(People Daily) alidokeza kuwa Msanii Otile Brown amemkopi kwa kuchukua model aliyefanya kazi naye kwa wimbo wake mpya Time. https://youtu.be/_pr9QRmGSzM "Niliambiwa kuwa Otile Brown hupenda kuigizia vitu mno na Nimeamini manake sasa nimejionea na hii imetokea pale Otile amefanya kazi na model niliyefanya kazi naye Mimi....." tukinukuu kauli yake Beka the Boy. Pande ya pili ya Msanii Otile Brown ilidokeza kuwa anayekopizia mwenzake ni Beka,kwani ana lazima kufuata nyayo za Otile Brown kwa kufanya Kazi na Dr Eddie. https://youtu.be/_pr9QRmGSzM

VIDEO MPYA YA MSANII MAREHEMU BENSO ALIYOKUWA AWACHIE..... ICHEKI HAPA

Image
Msanii Benso almaarufu Benson Katani japo hayupo nasi kwa sasa amewaachia wapenzi wa muziki wake video mpya kabisa.   Video hiyo kwa jina GOD'S PERFECT(akimshirikisha produza Petrooz) ilikua moja ya baadhi ya kazi zake alizokuwa na mikakati ya kuwachia mwaka huu kabla ya kukumbana na kifo chake.  Huku mashabiki na washika dau mbali mbali wakiwa katika hali ya majonzi na kuomboleza, video hiyo imeachiwa rasmi na mwandalizi Ricky Bekko wa Big Dreams. Rest in Peace Benso na hii hapa video yenyewe - https://youtu.be/eI16asEBrCE